MATOKEO:
Jumanne Februari 21
CSKA Moscow 1 Real Madrid 1
Napoli 3 Chelsea 1
TAARIFA:
Wakiwa huko Italia kwenye mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, Chelsea, kama wenzao Arsenal ambao ndio wawakilishi wa Ligi Kuu England waliobakia kwenye michuano hiyo baada ya Man United na Man City kutupwa nje, jana walitandikwa bao 3-1 na Napoli inayocheza Serie A.
Wiki iliyopita Arsenal ilikung’utwa bao 4-0 na AC Milan.
Jana Chelsea walitangulia kupata bao katika dakika ya 17 kwa bao la Juan Mata lakini Napoli walisawazisha dakika ya 38 kwa bao la Lavezzi na kuongeza bao la pili kupitia Edinson Cavani katika dakika ya 45.
Napoli walipata bao lao la 3 dakika ya 65 na alikuwa Lavezzi aliefunga tena.
Vikosi vilivyoanza:
Napoli: De Sanctis, Campagnaro, Cannavaro, Aronica, Maggio,
Inler, Gargano, Zuniga, Hamsik, Lavezzi, Cavani.
Akiba: Rosati, Grava, Dossena, Dzemaili, Fernandez, Pandev, Britos.
Chelsea: Cech, Ivanovic, Cahill, Luiz, Bosingwa, Ramires,
Meireles, Malouda, Sturridge, Drogba, Mata.
Akiba: Turnbull, Cole, Essien, Lampard, Torres, Mikel, Kalou.
Refa: Carlos Velasco Carballo [Spain]
RATIBA:
Jumatano Februari 22
[Saa 4 Dak 45 Usiku]
Basel v Bayern Munich
Marseille v Inter Milan