MATOKEO:
Jumapili Februari 19
Crawley 0 Stoke 2
Stevenage 0 Tottenham 0 [Kurudiana huko White Hart Lane-tarehe kutajwa baadae]
Liverpool 6 Brighton 1
TAARIFA:
Wakiwa kwao Anfield leo Liverpool wameifunga Brighton & Hoves, Timu ya Daraja la Championship ambalo liko chini ya Ligi Kuu England, kwa bao 6-1 na kutinga Robo Fainali ya FA Cup ambako watakuwa tena nyumbani Anfield kucheza na Stoke City.
Jumapili ijayo Februari 26, Liverpool wapo Wembley kucheza Fainali ya Carling Cup dhidi ya Cardiff City, Timu nyingine ya Daraja la chini la Championship.
Kati ya bao 6 walizopata Liverpool, bao 3 ni za kujifunga wenyewe kwa mabao ya Bridcutt, bao mbili, na Dunk, na mengine yalifungwa na wenyewe Liverpool kupitia Skrtel, Caroll na Suarez ambae pia alikosa penati.
Klabu nyingine ya Ligi Kuu, Tottenham, ikicheza ugenini na Timu ya Daraja la Ligi 1, Stevenage, ilitoka 0-0 na itabidi warudiane huko White Hart Lane ili kupata Mshindi atakaekuwa Uwanja wa nyumbani kwake kucheza na Bolton kwenye Robo Fainali.
MECHI ZA ROBO FAINALI:
Zitachezwa Wikiendi ya kuanzia Machi 7.
[Huenda zikachezwa Ijumaa, Jumamosi, Jumapili au pia Jumatatu]:
[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]
Liverpool v Stoke City
Chelsea au Birmingham v Leicester City
Tottenham au Stevenage v Bolton Wanderers
Everton v Sunderland