MATOKEO:
Jumatano Februari 15
Zenit 3 Benfica 2
AC Milan 4 Arsenal 0
TAARIFA:
Ni kweli hii ni Ligi ya Mabingwa maana leo ndani ya San Siro Mabingwa wa Italia AC Milan wamewatandika Arsenal, Timu ambayo Msimu uliopita ilimaliza nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England na kuingizwa kwenye michuano hii, kwa mabao 4-0 katika mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16.
Bao za AC Milan zilifungwa na Kevin Prince Boateng, Robinho, bao mbili, na Ibrahimovich kwa penati baada ya Djourou kuamua kucheza Raga badala ya Soka ndani ya boksi.
Bila shaka Arsenal watashukuru sana kufungwa bao 4 tu maana hii ilikuwa mechi ya upande mmoja na iliwachukua Arsenal dakika 66 mpaka kuweza kupiga shuti la kwanza golini kupitia Van Persie na kuokolewa na Kipa Abbiati.
Timu hizi zitarudiana Uwanjani Emirates hapo Machi 6
Vikosi:
AC Milan: Abbiati, Abate, Mexes, Thiago Silva, Antonini,
Seedorf, Van Bommel, Nocerino, Boateng, Ibrahimovic, Robinho.
Akiba: Amelia, Alexandre Pato, Nesta, Ambrosini, Bonera,
Emanuelson, El Shaarawi.
Arsenal: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Song, Rosicky, Walcott, Ramsey, Arteta, van Persie.
Akiba: Fabianski, Henry, Oxlade-Chamberlain, Djourou, Arshavin, Benayoun, Coquelin.
Refa: Viktor Kassai (Hungary)
RATIBA:
Jumanne Februari 21
CSKA Moscow v Real Madrid
Napoli v Chelsea
Jumatano Februari 22
Basel v Bayern Munich
Marseille v Inter Milan