Wakicheza kwao Uwanja wa Etihad huku wakiwa na ushindi wa bao 2-1 walioupata ugenini huko Ureno Wiki iliyopita, Manchester City leo walijihakikishia kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada ya kuishindilia FC Porto, ambao walikuwa ndio Mabingwa watetezi wa Kombe hili, kwa bao 4-0.
Bao za Man City zilifungwa na Sergio Aguero, Edin Dzeko, David Silva na David Pizarro.
Katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Man City wataanza kucheza ugenini na Mshindi kati ya Legia Warszawa ya Poland au Sporting Club ya Ureno ambao wanarudiana Alhamisi huko Ureno na matokeo ya mechi yao ya kwanza yalikuwa ni 2-2.
Katika Raundi hiyo ijayo Man City watamkosa Kiungo wao muhimu Yaya Toure kufuatia kupewa kwake Kadi ya Njano kwenye Dakika ya 65 katika mechi na FC Porto, hii ikiwa Kadi yake ya pili na hivyo kufungiwa mechi moja.
Maoni
Ndugu Robin,
Unachoweza kufanya ni kufungua website www.sokainbongo.com au ku-subscribe Facebook Page yetu ambayo ni https://www.facebook.com/pages/SOKA-in-Bongo/227579427269833