RATIBA/MATOKEO:
Jumanne Februari 21
CSKA Moscow 1 Real Madrid 1
[Saa 4 Dak 45 Usiku]
Napoli v Chelsea
TAARIFA:
Wakicheza ugenini huko Luzhniki Stadium iliyobanwa na kibaridi kikali kwenye mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano, Cristiano Ronaldo alipachika bao Dakika ya 28 na kuwapa Real Madrid bao la kuongoza lakini katika zile Dakika 3 za nyongeza mwishoni mwa Dakika 90, CSKA Moscow walimudu kusawazisha kufuatia kizaazaa golini kwa bao la Pontus Wernbloom kutoka Sweden.
Vikosi:
CSKA Moscow: 1-Sergei Chepchugov; 24-Vasily Berezutsky, 4-Sergei Ignashevich, 6-Alexei Berezutsky, 42-Georgy Shchennikov; 3-Pontus Wernbloom, 22-Yevgeny Aldonin, 21-Zoran Tosic, 10-Alan Dzagoyev; 8-Seydou Doumbia, 18-Ahmed Musa.
Real Madrid: 1-Iker Casillas; 17-Alvaro Arbeloa, 3-Pepe, 4-Sergio Ramos, 15-Fabio Coentrao; 6-Sami Khedira, 14-Xabi Alonso; 10-Mesut Ozil, 21-Jose Callejon, 7-Cristiano Ronaldo; 9-Karim Benzema.
RATIBA:
Jumatano Februari 22
[Saa 4 Dak 45 Usiku]
Basel v Bayern Munich
Marseille v Inter Milan