RATIBA/MATOKEO:
Nusu Fainali:
Januari 31
Mirandes 1 Athletic Bilbao 2
Februari 1
Valencia 1 Barcelona 1
Februari 7
Athletic Bilbao 6 Mirandes 2 [Athletic Bilbao imesonga kwa jumla ya mabao 8-3]
Februari 8
Barcelona 2 Valencia 0 [Barca imesonga kwa jumla ya mabao 3-1]
FAINALI=Mei 20 au 25
Athletic Bilbao v Barcelona
Taarifa:
Barcelona imejikita kwenye Fainali ya Kombe la Mfalme, Copa del Rey, baada ya kuichapa bao 2-0 Valencia Uwanjani Nou Camp katika mechi ya marudiano iliyochezwa jana.
Timu hizo zilitoka bao 1-1 katika mechi ya kwanza.
Barca itacheza Fainali na Athletic Bilbao ambao waliwabwaga Mirandes katika Nusu Fainali nyingine.
Mabao ya Barca yalifungwa na Cesc Fabregas katika dakika ya 16 na Xavi dakika ya 81.
Valencia walimaliza mechi hii wakiwa Mtu 10 baada ya Sofiane Feghouli kupewa Kadi Nyekundu katika dakika ya 77 baada ya kupata Kadi za Njano mbili.