Kwenye mechi mbili za mtoano wa FA Cup zilizochezwa jana, Klabu za Everton na Tottenham zimefanikiwa kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada ya kushinda mechi zao.
Tottenham, wakicheza ugenini, walifanikiwa kuitoa Timu ya Daraja la chini Watford kwa bao 1-0 na bao hilo la ushindi kufungwa na Rafael van der Vaart kwa shuti la mbali.
Katika mechi hiyo, Tottenham ambao walitwaa FA Cup kwa mara ya mwisho Mwaka 1991, waliwapumzisha Gareth Bale, Ledley King na Aaron Lennon.
Nao Everton waliifunga Fulham bao 2-1 kwa bao za Marouane Fellaini na Denis Stracqualursi huku bao la Fulham likifungwa na Danny Murphy kwa penati.
Michuano hii ya FA Cup inaendelea leo na kesho Jumapili.
FA CUP
RATIBA KAMILI:
[Saa 9 Mchana]
QPR v Chelsea
[Saa 9 Dak 45 Mchana]
Liverpool v Man United
[Saa 12 Jioni]
Blackpool v Sheffield Wed
Millwall v Southampton
Derby v Stoke
Hull v Crawley Town
Bolton v Swansea
Leicester v Swindon
Sheffield Utd v Birmingham
Stevenage v Notts County
West Brom v Norwich
[Saa 2 na Robo Usiku]
Brighton v Newcastle
Jumapili Januari 29
[Saa 10 na Nusu jioni]
Sunderland v Middlesbrough
[Saa 1 Usiku]
Arsenal v Aston Villa
=========
LIGI KUU England
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumanne, 31 January 2012
[Saa 4 Dak 45 Usiku]
Swansea v Chelsea
Tottenham v Wigan
Wolverhampton v Liverpool
[Saa 5 Usiku]
Bolton v Arsenal
Man United v Stoke
Sunderland v Norwich
Jumatano, 1 February 2012
[Saa 4 Dak 45 Usiku]
Aston Villa v QPR
[Saa 5 Usiku]
Blackburn v Newcastle
Everton v Man City
Fulham v West Brom

![]() |