Jose Mourinho amedai kuwa baadhi ya Wachezaji wake wa Real Madrid wana imani kuwa hawawezi kushinda Nou Camp licha ya jana kutoka nyuma kwa bao 2-0 na kumaliza mechi wakiwa 2-2 na Barcelona lakini wakatolewa nje ya Copa del Rey kwa vile walifungwa mechi ya kwanza 2-1.
Licha ya kutawala kipindi cha kwanza, Real walijikuta wakipigwa bao mbili katika dakika ya 43 na Pedro na ya 45 na Daniel Alves lakini wakasawazisha kwa bao za Ronaldo, dakika ya 68 na Karim Benzema dakika ya 72.
Imani hiyo kutokuweza kushinda Nou Camp ya Wachezaji wa Real imekuja baada ya Refa wa pambano lao la jana kuwapa Wachezaji wa Real Kadi za Njano 8 mbili zikiwa kwa Sergio Ramos alietolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Mourinho alihoji ikiwa Timu ngeni zinapocheza Nou Camp nyumbani kwa Barcelona kama zinatendewa haki na Marefa na aliongeza: ‘Nimecheza hapa na Chelsea, Inter Milan na Real na hili si jipya! Nitawapa hongera Barca kwa kile walichofanya Bernabeu Wiki iliyopita lakini si kwa mechi hii au kwenda Nusu Fainali.’
Nae Meneja wa Barcelona, Pep Guardiola, hakutaka kujiingiza kwenye ubishi huo ila alisema ameshukuru kuingia Nusu Fainali ya Copa del Rey.
Guardiola pia alitamka: ‘Real ni Timu ngumu na ushindi huu ni pongezi kwetu. Sasa ni vigumu kuifunga Real kupita ilivyokuwa na kufuzu huku kumetufanya tuwe na furaha!’

![]() |
Maoni