UWANJANI ULAYA

Barca v Real=Copa del Rey: Pepe kucheza akiwa fiti – Mourinho

Jumanne, 24 Januari 2012 18:48
Chapisha Toleo la kuchapisha

EL_CLASICO_PART_1Beki wa Real Madrid Pepe atacheza kwenye mechi ya marudiano ya Copa del Rey itakayochezwa Jumatano Uwanjani Nou Camp ikiwa yuko fiti licha ya kuzua mgogoro mkubwa baada ya kumkanyaga mkononi Lionel Messi katika mechi ya kwanza ya Kombe hilo iliyochezwa Wiki iliyopita huko Santiago Bernabeu na Real kuchapwa 2-1 na Barca.JOSE_MOURINHO

Refa katika mechi hiyo ambayo Pepe alimkanyaga Messi hakuona tukio hilo na wengi walitegemea Shirikisho la Soka la Spain, RFEF, litamwadhibu Mreno huyo lakini jana waliamua kutomchukulia hatua yeyote.

Pepe hakuwemo kwenye Kikosi cha Real kilichoifunga Atletic Bilbao bao 4-1 majuzi Jumapili lakini leo Kocha wa Real Jose Mourinho amethibitisha ikiwa Pepe, ambae ameumia pamoja na Viungo Lassana Diarra na Esteban Granero, watakuwa fiti atawachezesha.

Mourinho, akiongea na Wanahabari hivi leo, alikwepa kujibu maswali yaliyohusiana na mbinu atakazotumia ili kuifunga Barca Timu ambayo imemfunga mara 5 kati ya 9 alizocheza nao tangu atue Real na kuambulia kushinda mara moja tu kwa bao 1-0 alilofunga Cristiano Ronaldo kwenye Fainali ya Copa del Rey Msimu uliopita walipotwaa Kombe hilo.

Hata hivyo, kama kawaida yake Mourinho hakuacha majigambo kwa kukumbusha kwenye La Liga wanaongoza wakiwa pointi 5 mbele ya Barca pale alipotamka: ‘Tuko pointi 5 mbele ya Timu ambayo kila Mtu anadai ni bora Duniani!’

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2
SOKAINBONGO_BANNER1