Mashindano makubwa ya Klabu za Ulaya yataingia tena dimbani katikati ya Wiki hii kwa UEFA CHAMPIONZ LIGI kuchezwa Jumanne na Jumatano mechi zake zilizobaki za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na EUROPA LIGI kuchezwa mechi za marudiano ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 hapo Jumatano na Alhamisi.
Wakongwe wa Ligi Kuu England, Chelsea, wao wapo ugenini huko Italia hapo Jumanne kucheza na Napoli kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI na siku hiyo hiyo kwenye michuano hiyo Magwiji wa Ulaya, Real Madrid ya Spain watakuwa ugenini huko Urusi kucheza na CSKA Moscow.
Jumatano kutakuwa na mechi mbili za UEFA CHAMPIONZ LIGI na moja ya EUROPA LIGI ambayo Manchester City watakuwa kwao Etihad kurudiana na Mabingwa watetezi FC Porto ambao Wiki iliyopita huko Ureno waliwafunga bao 2-1.
Alhamisi Februari 23 zitachezwa mechi nyingine 15 zilizobaki za EUROPA LIGI na miongoni mwake ni Magwiji Manchester United kuwa kwao Old Trafford kurudiana na Ajax Amsterdam ambayo waliichapa 2-0 Wiki iliyopita.
RATIBA:
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Jumanne Februari 21
CSKA Moscow v Real Madrid
Napoli v Chelsea
Jumatano Februari 22
Basel v Bayern Munich
Marseille v Inter Milan
EUROPA LIGI:
[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]
Jumatano Februari 22
[Saa 2 Usiku]
Manchester City v FC Porto [2-1]
Alhamisi Februari 23
[Saa 3 Usiku]
Athletic Bilbao v Lokomotiv Moscow [1-2]
PSV Eindhoven v Trabzonspor [2-1]
Standard Liege v Wisla Krakow [1-1]
Club Brugge v Hannover [1-2]
Valencia v Stoke City [1-0]
Twente v Steaua Bucharest [1-0]
Paok Salonika v Udinese [0-0]
Metalist Kharkiv v Red Bull Salzburg [4-0]
[Saa 5 Dak 5 Usiku]
Olympiakos v Rubin Kazan [1-0]
Manchester United v Ajax [2-0]
Atlético Madrid v Lazio [3-1]
Besiktas v Sporting Braga [2-0]
Anderlecht v AZ Alkmaar [0-1]
Sporting Lisbon v Legia Warsaw [2-2]
Schalke v Viktoria Plzen [1-1]
RAUNDI YA MTOANO TIMU 16:
Mechi kuchezwa Machi 8 na marudio Machi 15
[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]
FC Salzburg/Metalist Kharkiv v Rubin Kazan v Olympiacos
Legia Warszawa/Sporting Club v FC Porto/Manchester City
Steaua Bucuresti/FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke
AZ Alkmaar/Anderlecht v Udinese/PAOK
Stoke City/Valencia v Trabzonspor/PSV Eindhoven
Ajax Amsterdam/Manchester United v Lokomotiv Moscow/Athletic Bilbao
Steaua Bucuresti /FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke
Wisla Krakow/Standard Liege v Hannover 96/Brugge