♦ Awa Supastaa kwenye Intaneti!
Paka ambae jana aliingia Uwanjani Anfield wakati mechi ya Ligi Kuu England kati ya Liverpool na Tottenham ikichezwa na kusababisha mechi hiyo isimame kwa Dakika 3 amepata umaarufu mkubwa mtandaoni na kuna akaunti kadhaa za Twitter zimeanzishwa kwa ajili yake.
Mojawapo wa akaunti hizo za Twitter, @AnfieldCat, hadi mapema leo ilikuwa imeshapata Mashabili 17,368 huku video za Paka huyo zikiwa kivutio kikubwa mtandaoni.
Katika posti moja ya hiyo Twitter, iliandikwa: ‘Everton wanataka kunisaini na Mmiliki wao Bill Kenwright atatoa dau kuninunua!’ hii ikiwa kuwadhihaki Mahasimu wakubwa wa Liverpool Klabu ya Everton ambao pia wapo Jijini Liverpool.
Katika mechi hiyo Liverpool na Tottenham zilitoka sare ya 0-0.