SOKA SPESHO

CARLING CUP: Cardiff yatinga Fainali kwa matuta!

Jumatano, 25 Januari 2012 09:04
Chapisha Toleo la kuchapisha

RATIBA/MATOKEO:

Jumanne, Januari 24

Cardiff City 1 Crystal Palace 0 (Jumla ya Magoli 1-1, Cardiff wapita kwa penati 3-1)

Jumatano, Januari25

Liverpool v Man City (Jumla ya Magoli 1-0)

FAINALI

Jumapili Februari 26

Cardiff City v Liverpool/Man City

TAARIFA:

Kipa wa Cardiff City Tom Heaton, ambae ametokea Timu ya Vijana ya Manchester United, jana alikuwa shujaa mkubwa kwa kuokoa penati mbili na kuibeba Timu yake kwenda Wembley kwenye Fainali ya Carling Cup wakati walipopigiana mikwaju ya penati tano tano baada ya kwenda sare ya jumla ya bao 1-1 katika mechi mbili na Crystal Palace.

Crystal Palace walishinda mechi ya kwanza ya Nusu Fainali kwa bao 1-0 lililofungwa na Anthony Gardner na jana Anthony Gardner alifunga tena bao, bao la kujifunga mwenyewe katika dakika ya 7, na kuwapa ushindi Cardiff City wa bao 1-0.

Kwa vile jumla ya mabao ilikuwa 1-1 katika mechi mbili Timu hizi zilipelekwa kwenye dakika 30 za nyongeza huku Crystal Palace wakicheza Mtu 10 baada ya McCarthy kutolewa kwa Kadi Nyekundu kwenye dakika ya 78.

Hadi dakika 120 zinamalizika mabao yalibaki 1-1 na ndipo ikaja tombola ya mikwaju ya penati ambazo Kipa Tom Heaton aliokoa mbili na Cardiff City kuishinda Crystal Palace kwa penati 3-1.

Cardiff City imetinga Fainali na inamngoja mshindi wa mechi ya leo kati ya Liverpool na Man City huku Liverpool wakiwa wameshinda bao 1-0 katika mechi ya kwanza.

Fainali hiyo itachezwa Uwanja wa Wembley Jijini London hapo Februari 26.

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2
SOKAINBONGO_BANNER1