SOKA SPESHO

EUROPA LIGI: Man United kusonga?

Jumatano, 22 Februari 2012 21:23
Chapisha Toleo la kuchapisha

Man_United_v_AjaxManchester United v Ajax Amsterdam [Matokeo Mechi ya kwanza 2-0]

UWANJA: Old Trafford

SAA: 5 Dakika 5 Usiku

TAARIFA:

Manchester United Alhamisi usiku wanaikaribisha Ajax Amsterdam ya Uholanzi Uwanjani Old Trafford katika mechi ya marudiano ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya EUROPA LIGI baada ya kuifunga Ajax bao 2-0 huko Amsterdam ArenA Wiki iliyopita.

Mshindi wa mechi hii atapambana na Mshindi wa Mechi kati ya Athletic Bilbao na Lokomotiv Moscow kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na matokeo ya mechi ya Timu hizi katika mechi yao ya kwanza yalikuwa ni Lokomotiv Moscow 2 Athletic Bilbao 1 kwenye mechi iliyochezwa huko Urusi Wiki iliyopita.

HALI YA TIMU:

Baada ya kusuasua kwenye Msimu huu wa Ligi yao huko Uholanzi, Eredivisie, Ajax wamefanikiwa kushinda mechi yao ya pili mfululizo kwa kuichapa NEC Nijmegen bao 4-1 Wikiendi iliyopita.

Lakini, Ajax, wakiwa chini wa nguli wa Soka la Uholanzi, Frank De Boer, bila shaka, wanajua fika kuwa baada ya kuchapwa bao 2-0 huko kwao nafasi yao kusonga iko finyu katika mechi yao dhidi ya Man United Old Trafford.

Tangu mechi yao huko Amsterdam ArenA, Man United hawajacheza mechi yeyote kwa vile Wikiendi iliyopita kulikuwa ni mechi za FA Cup tu na wao walishatupwa nje ya michuano hiyo.

WACHEZAJI:

Staa wa Man United Wayne Rooney hatakuwepo kwa vile ni mgonjwa lakini Dimitar Berbatov huenda akacheza baada ya kupona maumivu huku kuna tetesi Kiungo chipukizi Paul Pogba huenda akapewa namba pamoja na kina Chris Smalling na Tom Cleverley.

Ajax itawakosa Nicolai Boilesen, Dmitry Bulykin na Theo Janssen lakini Beki wa zamani wa Blackburn, Andre Ooijer, anaweza kupewa namba.

REFA:

Damir Skomina ndie Mwamuzi na ndie aliechezesha mechi ambayo Napoli waliwafunga Manchester City 2-1 mapema Msimu huu kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI.

RATIBA:

[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]

Alhamisi Februari 23

[Saa 3 Usiku]

Athletic Bilbao v Lokomotiv Moscow [1-2]

PSV Eindhoven v Trabzonspor [2-1]

Standard Liege v Wisla Krakow [1-1]

Club Brugge v Hannover [1-2]

Valencia v Stoke City [1-0]

Twente v Steaua Bucharest [1-0]

Paok Salonika v Udinese [0-0]

Metalist Kharkiv v Red Bull Salzburg [4-0]

[Saa 5 Dak 5 Usiku]

Olympiakos v Rubin Kazan [1-0]

Manchester United v Ajax [2-0]

Atlético Madrid v Lazio [3-1]

Besiktas v Sporting Braga [2-0]

Anderlecht v AZ Alkmaar [0-1]

Sporting Lisbon v Legia Warsaw [2-2]

Schalke v Viktoria Plzen [1-1]

RAUNDI YA MTOANO TIMU 16:

Mechi kuchezwa Machi 8 na marudio Machi 15

[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]

FC Salzburg/Metalist Kharkiv v Rubin Kazan v Olympiacos

Legia Warszawa/Sporting Club v FC Porto/Manchester City

Steaua Bucuresti/FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

AZ Alkmaar/Anderlecht v Udinese/PAOK

Stoke City/Valencia v Trabzonspor/PSV Eindhoven

Ajax Amsterdam/Manchester United v Lokomotiv Moscow/Athletic Bilbao

Steaua Bucuresti /FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

Wisla Krakow/Standard Liege v Hannover 96/Brugge

 

NI UEFA TENA-CHAMPIONZ LIGI na EUROPA LIGI kati ya Wiki

Jumapili, 19 Februari 2012 22:10
Chapisha Toleo la kuchapisha

UEFA_ULAYAMashindano makubwa ya Klabu za Ulaya yataingia tena dimbani katikati ya Wiki hii kwa UEFA CHAMPIONZ LIGI kuchezwa Jumanne na Jumatano mechi zake zilizobaki za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na EUROPA LIGI kuchezwa mechi za marudiano ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 hapo Jumatano na Alhamisi.

Wakongwe wa Ligi Kuu England, Chelsea, wao wapo ugenini huko Italia hapo Jumanne kucheza na Napoli kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI na siku hiyo hiyo kwenye michuano hiyo Magwiji wa Ulaya, Real Madrid ya Spain watakuwa ugenini huko Urusi kucheza na CSKA Moscow.

Jumatano kutakuwa na mechi mbili za UEFA CHAMPIONZ LIGI na moja ya EUROPA LIGI ambayo Manchester City watakuwa kwao Etihad kurudiana na Mabingwa watetezi FC Porto ambao Wiki iliyopita huko Ureno waliwafunga bao 2-1.

Alhamisi Februari 23 zitachezwa mechi nyingine 15 zilizobaki za EUROPA LIGI na miongoni mwake ni Magwiji Manchester United kuwa kwao Old Trafford kurudiana na Ajax Amsterdam ambayo waliichapa 2-0 Wiki iliyopita.

RATIBA:

UEFA CHAMPIONZ LIGI

Jumanne Februari 21

CSKA Moscow v Real Madrid

Napoli v Chelsea

Jumatano Februari 22

Basel v Bayern Munich

Marseille v Inter Milan

EUROPA LIGI:

[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]

Jumatano Februari 22

[Saa 2 Usiku]

Manchester City v FC Porto [2-1]

Alhamisi Februari 23

[Saa 3 Usiku]

Athletic Bilbao v Lokomotiv Moscow [1-2]

PSV Eindhoven v Trabzonspor [2-1]

Standard Liege v Wisla Krakow [1-1]

Club Brugge v Hannover [1-2]

Valencia v Stoke City [1-0]

Twente v Steaua Bucharest [1-0]

Paok Salonika v Udinese [0-0]

Metalist Kharkiv v Red Bull Salzburg [4-0]

[Saa 5 Dak 5 Usiku]

Olympiakos v Rubin Kazan [1-0]

Manchester United v Ajax [2-0]

Atlético Madrid v Lazio [3-1]

Besiktas v Sporting Braga [2-0]

Anderlecht v AZ Alkmaar [0-1]

Sporting Lisbon v Legia Warsaw [2-2]

Schalke v Viktoria Plzen [1-1]

RAUNDI YA MTOANO TIMU 16:

Mechi kuchezwa Machi 8 na marudio Machi 15

[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]

FC Salzburg/Metalist Kharkiv v Rubin Kazan v Olympiacos

Legia Warszawa/Sporting Club v FC Porto/Manchester City

Steaua Bucuresti/FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

AZ Alkmaar/Anderlecht v Udinese/PAOK

Stoke City/Valencia v Trabzonspor/PSV Eindhoven

Ajax Amsterdam/Manchester United v Lokomotiv Moscow/Athletic Bilbao

Steaua Bucuresti /FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

Wisla Krakow/Standard Liege v Hannover 96/Brugge

 

EUROPA LIGI: Klabu za Manchester zashinda ugenini, Stoke hoi nyumbani!

Ijumaa, 17 Februari 2012 09:11
Chapisha Toleo la kuchapisha

AJAX_v_MAN_UNITED_EUROPA14Manchester United wakicheza ugenin huko Amsterdam ArenA jana waliwafunga Ajax Amsterdam bao 2-0 huku Mahasimu wao Manchester City wakishinda huko Ureno kwa bao 2-1 dhidi ya Mabingwa watetezi FC Porto lakini wenzao wa Ligi Kuu Stoke City, wakiwa nyumbani, walichapwa bao 1-0 na Valencia.

Mabao ya Man United yalifungwa na Ashley Young na Javier Hernandez ‘Chicharito’.

Man City walitanguliwa bao moja na FC Porto lakini wakasawazisha kwa bao la Alvaro Pereira aliejifunga mwenyewe na Sergio Aguero kupiga bao la pili.

Man City watarudiana na FC Porto Uwanjani Etihad hapo Februari 22 na Man United kucheza na Ajax Uwanjani Old Trafford hapo Februari 23.

MATOKEO KAMILI:

Jumanne Februari 14

Rubin Kazan 0 Olympiacos 1

SC Braga 0 Besiktas 2

Alhamisi Februaru 16

FC Porto 1 Manchester City 2

Ajax Amsterdam 0 Manchester United 2

Lokomotiv Moscow 2 Athletic Bilbao 1

FC Salzburg 0 Metalist Kharkiv 4

Stoke City 0 Valencia 1

AZ Alkmaar 1 Anderlecht 0

Lazio 1 Atletico Madrid 3

Steaua Bucuresti 0 FC Twente 1

Viktoria Plzen 1 Schalke 1

Wisla Krakow 1 Standard Liege 1

Udinese 0 PAOK 0

Trabzonspor 1 PSV Eindhoven 2

Hannover 2 Brugge 1

Legia Warszawa 2 Sporting Club 2

 

EUROPA LIGI: Ajax v Man United Alhamisi usiku!

Jumatano, 15 Februari 2012 20:33
Chapisha Toleo la kuchapisha

AJAX_v_MAN_UNITED_EUROPA14UWANJA: Amsterdam ArenA

TAIMU: Saa 3 Usiku Bongo Taimu

Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya EUROPA Cup ilianza jana kwa mechi mbili na inaendelea kesho kwa mechi nyingine 14 huku Klabu za Jiji la Manchester ambazo ndizo zipo kileleni mwa Ligi Kuu England zikicheza ugenini.

Manchester City wao wako huko Ureno kuwavaa Mabingwa watetezi wa Kombe hili FC Porto na Mabingwa wa England, Manchester United, wao wapo Amsterdam kucheza na Ajax Amsterdam kwenye Uwanja wa Amsterdam ArenA.

Timu ya tatu ya England kucheza kwenye michuano hii ni Stoke City ambao watakuwa nyumbani kucheza na Valencia ya Spain.

Mbali ya ile dhana kuwa michuano hii si mikubwa lakini ukweli ni kuwa Kombe hili si la kubeza hasa ukizichukulia Timu nzito na zenye historia huko Ulaya ambazo zimo kwenye michuano hii kama vile Ajax, Porto na Man United, ambao kati yao wameshatwaa Mataji ya Ulaya mara 14.

Man City wao walishinda Taji moja tu na hiyo ilikuwa zaidi ya Miaka 40 iliyopita pale Mwaka 1970 walipotwaa Kombe la wakati huo Kombe la Washindi.

Hata hivyo, Meneja wa Man United, Sir Alex Ferguson, amesisitiza: ‘Silidharau Kombe hili. Bado ni Kombe la Ulaya na kuna kiwango kizuri humo. Pia hatujawahi kulitwaa!’

TAARIFA=Ajax v Man United

Ajax na Man United zimewahi kukutana mara 3 katika michuano mikubwa na mara ya mwisho ilikuwa ni kwenye Raundi ya kwanza ya Kombe la Ulaya Mwaka 1976/77 na Ajax kushinda bao 1-0 lakini kwenye mechi ya marudiano huko Old Trafford Man United walishinda bao 2-0 kwa bao za Lou Macari na Sammy McIlroy.

Ajax waliwahi kuwika Miaka ya nyuma na mara ya mwisho kutwaa Taji Ulaya ilikuwa Mwaka 1995 walipotwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI lakini Msimu huu, ingawa ni Mabingwa watetezi, wanasuasua kwenye Ligi yao Eredivisie na wapo nafasi ya 6.

Mwaka huu Ajax wameshinda mechi moja tu na tena ni Wikiendi iliyopita walipoipiga NAC Breda 2-0 kwenye Ligi lakini wapinzani wao Man United wameshinda mechi 5 kati ya 8 zikiwemo zile za ugenini dhidi ya Man City na Arsenal

Refa:

Ni Gianluca Rocchi kutoka Italy ambae Msimu huu ameshatembeza Kadi za Njano 62 na Nyekundu 2 kwenye gemu 14 alizochezesha zikiwemo mbili za UEFA CHAMPIONZ LIGI za Arsenal, kwenye sare ya ugenini 1-1 na Borussia Dortmund, na ile ya Chelsea iliyochezwa Stamford Bridge na wao kuishinda Valencia 3-0.

Kikosi cha Man United kilichosafiri:

De Gea, Amos; Fabio, Rafael, Evans, Jones, Smalling, Fryers, Ferdinand; Valencia, Nani, Carrick, Young, Park, Scholes, Cleverley, Pogba; Rooney, Hernandez, Welbeck.

Fahamu: Giggs, Evra na Berbatov hawakusafiri

EUROPA LIGI:

Raundi ya Pili ya Mtoano:

Jumanne Februari 14

Rubin Kazan 0 Olympiacos 1

SC Braga 0 Besiktas 2

Alhamisi Februaru 16

FC Porto v Manchester City

Ajax Amsterdam v Manchester United

Lokomotiv Moscow v Athletic Bilbao

FC Salzburg v Metalist Kharkiv

Stoke City v Valencia

AZ Alkmaar v Anderlecht

Lazio v Atletico Madrid

Steaua Bucuresti v FC Twente

Viktoria Plzen v Schalke

Wisla Krakow v Standard Liege

Udinese v PAOK

Trabzonspor v PSV Eindhoven

Hannover 96 v Brugge

Legia Warszawa v Sporting Club

 

LISTI UBORA DUNIANI: Spain bado 1, Zambia ndani 50 bora, Bongo chini—ipo 139!

Jumatano, 15 Februari 2012 13:04
Chapisha Toleo la kuchapisha

FIFA-logo-300Wakati Mabingwa wa Dunia na Ulaya, Spain, bado wameendelea kushikilia nafasi ya kwanza, Mabingwa wapya wa Afrika, Zambia, wamepanda nafasi 28 na sasa wapo nafasi ya 43 katika Listi ya FIFA/Coca Cola ya Ubora Duniani iliyotolewa leo.

Tanzania imezidi kuporomoka kwa kushuka nafasi mbili na sasa ipo nafasi ya 139.

Ingawa walifungwa na Zambia kwenye Fainali ya AFCON, Ivory Coast imebaki ndiyo Timu ya juu kabisa toka Afrika na inashikilia nafasi ya 15 baada ya kupanda nafasi mbili.

Katika 10 bora, Germany imepanda nafasi moja na ipo nafasi ya pili na Argentina imetupwa nje ya 10 bora na Denmark ambao wamechukua nafasi ya 10.

Listi nyingine ya FIFA/Coca Cola ya Ubora Duniani itatolewa hapo tarehe 7 Machi 2012.

KUMI BORA:

1 Spain

2 Germany

3 Netherlands

4 Uruguay

5 England

6 Portugal

7 Brazil

8 Italy

9 Croatia

10 Denmark

 


Page 1 of 47

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2
SOKAINBONGO_BANNER1