SOKA LA DUNIA

UEFA CHAMPIONZ LIGI: Barca yashinda ugenini!

Jumatano, 15 Februari 2012 07:44
Chapisha Toleo la kuchapisha

BARCA_MAFANIKIOMATOKEO:

Jumanne Februari 14

Bayer Leverkusen 1 FC Barcelona 3

Lyon 1 Apoel Nicosia 0

TAARIFA:

Bao mbili za Fowadi kutoka Chile Alexis Sanchez zimeisaidia Barcelona, Mabingwa watetezi wa Ulaya, kuishinda kwa bao 3-1 Bayer Leverkusen huko Ujerumani katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI iliyochezwa jana usiku.

Sanchez alifunga bao la kwanza dakika ya 41 na la pili dakika ya 55.

Bayer Leverkusen walipata bao lao dakika ya 52 kupitia Michal Kadlec na kuifanya gemu iwe 1-1 wakati huo.

Bao la 3 la Barcelona lilifungwa dakika ya 88 na Lionel Messi.

Timu hizi zitarudiana hapo Machi 7.

Lyon 1 APOEL Nicosia 0

Katika mechi nyingine ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI iliyochezwa huko Ufaransa, Lyon iliwachapa Apoel Nicosia ya Cyprus kwa bao 1-0 kwa bao la dakika ya 58 la Alexandre Lacazette.

RATIBA:

[Mechi ni Saa 4 Dak 45 Usiku isipokuwa inapotajwa]

Jumatano Februari 15

Zenit v Benfica [Saa 2 Usiku]

AC Milan v Arsenal

Jumanne Februari 21

CSKA Moscow v Real Madrid

Napoli v Chelsea

Jumatano Februari 22

Basel v Bayern Munich

Marseille v Inter Milan

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

adidas

All Originals 300x250

MATANGAZO

TANGAZA HAPA