♣Man United 2 Liverpool 1
Bao mbili za Wayne Rooney katika dakika ya 47 na 50 yamewapa Manchester United ushindi wa bao 2-1 walipowachapa wapinzani wao wakubwa Uwanjani Old Trafford na kutwaa uongozi wa Ligi Kuu England wakiwa pointi moja mbele ya Mahasimu wao wengine Man City ambao kesho wako ugenini kucheza na Aston Villa.
+++++++
MSIMAMO:
1 Man United 58
2 Man City Pointi Pointi 57
3 Tottenham 50
4 Chelsea 43
-----------------------------------
5 Newcastle 42
6 Arsenal 40
7 Liverpool 39
+++++++
Mechi hii iligubikwa na mzozo uliohusu Straika wa Liverpool Luis Suarez kufungiwa mechi 8 kwa kumtukana kibaguzi Patrice Evra katika mechi yao ya kwanza ya Ligi na leo ilikuwa mara ya kwanza kwa Suarez kukutana uso kwa uso na Evra lakini inaelekea Suarez bado anataka kuendelea na bifu hilo pale alipokataa kumpa mkono Evra kabla mechi kuanza licha ya Evra kumshika mkono na hilo lilimfanya Rio Ferdinand akatae kumpa mkono Suarez.
Bao la Liverpool lilifungwa na Suarez katika Dakika ya 80.
Vikosi:
Man United De Gea; Rafael, Ferdinand, Evans, Evra; Valencia, Carrick, Scholes, Giggs; Rooney, Welbeck
Akiba: Amos, Fabio, Cleverley, Park, Pogba, Berbatov, Hernandez
Liverpool: Reina, Johnson, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Spearing, Henderson, Kuyt, Gerrard, Downing, Suarez
Akiba: Doni, Carroll, Carragher, Adam, Shelvey, Kelly, Bellamy.
Refa: Phil Dowd
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi Februari 11
Manchester United 2 Liverpool 1
Saa 12 Jioni
Bolton Wanderers v Wigan Athletic
Sunderland v Arsenal
Blackburn Rovers v QPR
Swansea City v Norwich City
Everton v Chelsea
Fulham v Stoke City
Saa 2 na Nusu Usiku
Tottenham v Newcastle United