RATIBA:
Jumamosi Februari 11
Saa 9 Dak 45 Mchana
Manchester United v Liverpool
Saa 12 Jioni
Bolton Wanderers v Wigan Athletic
Sunderland v Arsenal
Blackburn Rovers v QPR
Swansea City v Norwich City
Everton v Chelsea
Fulham v Stoke City
Saa 2 na Nusu Usiku
Tottenham v Newcastle United
Taarifa:
Manchester United v Liverpool
Siku zote hii ni mechi kubwa inayovutia wengi kila kona ya Dunia na leo ipo Uwanjani Old Trafford.
Hali za Vikosi:
Kiungo mahiri, chipukizi Tom Cleverly, atakuwemo kwenye Kikosi cha Man United baada ya kupona maumivu ya enka yaliyomweka nje kwa Miezi mitatu.
Lakini Man United watamkosa Beki Phil Jones ambae ni majeruhi ingawa mwenzake Chris Smalling amepona na huenda akachezeshwa.
Straika wa Liverpool Luis Suarez huenda akaanza mechi yake ya kwanza tangu atoke kifungo cha mechi 8 kwa kumkashifu kibaguzi Beki wa Man United Patrci Evra na leo watakutana uso kwa uso na huenda leo wakapeana mikono kabla mechi kuanza wakati Timu zinaposalimiana.
Uso kwa Uso:
Katika mechi 7 za mwisho kuchezwa Old Trafford kati ya Timu hizi, Man United wameshinda mechi 6 na Liverpool mara moja tu hiyo ikiwa ni Machi 2009.
Everton v Chelsea
Hii mechi inachezwa Uwanja wa Goodison Park kuanzia Saa 12 Jioni mara baada ya Man United kuivaa Liverpool.
Hali za Vikosi:
Mfungaji mahiri wa Everton Tim Cahill huenda akacheza baada ya kupona maumivu yake na pia Mchezaji mpya Nkica Jelavic huenda akaichezea Everton mechi yake ya kwanza Uwanjani Goodison Park.
Everton itawakosa Phil Jagielka, Leon Osman, Jack Rodwell na Seamus Coleman ambao ni majeruhi.
Chelsea huenda wakawa na Viungo Frank Lampard na John Obi Mikel baada ya kupona maumivu yao na Ashley Cole atarudi baada ya kutumikia kifungo cha mechi moja.
Uso kwa Uso:
Katika mechi mbili za mwisho kwa Chelsea kucheza Goodison Park wamefungwa mechi zote.
Sunderland v Arsenal
Hali za Vikosi:
Wachezaji wapya wa Sunderland, Wayne Bridge na Sotirios Kyrgiakos, ambao wapo hapo kwa mkopo wanaweza kucheza mechi yao ya kwanza.
Nicklas Bendtner, ambae yupo kwa mkopo Sunderland kutoka Arsenal, leo haruhusiwi kucheza kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu zinazokataza Mchezaji alie kwa mkopo kucheza dhidi ya Klabu yake iliyomwajiri.
Fulbeki wa Arsenal, Kieran Gibbs, huenda akaonekana leo baada ya kupona nyonga iliyokuwa imemuweka nje tangu mwanzoni mwa Oktoba.
Uso kwa Uso:
Arsenal hawajafungwa na Sunderland katika mechi zao 4 za mwisho walizocheza Stadium of Light lakini kati ya hizo 3 zilikuwa ni sare.
Tottenham v Newcastle United
Hali za Vikosi:
Tottenham itawakaribisha tena Jermain Defoe na Aaron Lennon waliopona maumivu yao lakini itawakosa majeruhi Ledley King, Younes Kaboul, Rafael van der Vaart na Sandro.
Baada ya kuikosa mechi iliyopita Tottenham waliposafiri kwenda kucheza na Liverpool kufuatia Ndege yake kufutiwa safari kwa ajili ya hali ya hewa mbaya, Meneja wa Tottenham Harry Redknapp leo atakuwepo Uwanjani White Hart Lane.
Uso kwa Uso:
Newcastle wamewafunga Tottenham 3-2 Msimu wa 2006/7 na 4-1 Msimu uliofuatia lakini baada ya hapo wamefungwa mechi mbili mfululizo hapo White Hart Lane.
MECHI ZIJAZO:
Jumapili Februari 12
Saa 10 na Nusu Jioni
Wolves v West Bromwich
Saa 1 Usiku
Aston Villa v Man City
[Timu zimecheza Mechi 24]
1 Man City Pointi Pointi 57
2 Man United 55
3 Tottenham 50
4 Chelsea 43
-----------------------------------
5 Newcastle 42
6 Arsenal 40
7 Liverpool 39
8 Sunderland 33
9 Norwich 32
10 Swansea 30
11 Everton 30
12 Stoke City 30
13 Aston Villa 28
14 Fulham 27
15 WBA 26
16 QPR 21
17 Wolves 21
--------------------------------
18 Bolton 20
19 Blackburn 18
20 Wigan 15