RATIBA:
Jumamosi Februari 11
Saa 9 Dak 45 Mchana
Manchester United v Liverpool
Saa 12 Jioni
Bolton Wanderers v Wigan Athletic
Sunderland v Arsenal
Blackburn Rovers v QPR
Swansea City v Norwich City
Everton v Chelsea
Fulham v Stoke City
Saa 2 na Nusu Usiku
Tottenham v Newcastle United
Bila shaka Wikiendi hii mimacho ya Wadau wengi wa Soka itakuwa Old Trafford kushuhudia Mabingwa Manchester United wakiwakwaa Mahasimu wao wa enzi na enzi Liverpool huku vivutio vikubwa kwenye mechi hii vikiwa kwanza hii ni BIGI MECHI, pili ushindi kwa Man United utawafanya watwae uongozi wa Ligi kwa vile vinara Man City wanacheza Siku inayofuata na tatu hii itakuwa mara ya kwanza kwa Patrice Evra kukutana na Luis Suarez tangu Straika huyo wa Liverpool kutoka kifungo cha Mechi 8 kwa kumkashifu kibaguzi Evra kwenye mechi ya Ligi iliyochezwa huko Anfield mapema Msimu huu.
++++++++++++++++++
MSIMAMO Timu za juu:
[Timu zimecheza Mechi 24]
1 Man City Pointi Pointi 57
2 Man United 55
3 Tottenham 50
4 Chelsea 43
-----------------------------------
5 Newcastle 42
6 Arsenal 40
7 Liverpool 39
++++++++++++++++++
Mbali ya hayo, hii ni mechi muhimu kwa Liverpool ambao wapo nafasi ya 7 na wako pointi 4 nyuma ya Chelsea waliokamata nafasi lulu ya 4 katika msimamo wa Ligi ikiwa ndiyo nafasi ya mwisho kwa Timu kupata fursa kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao.
Juu ya Liverpool wapo Arsenal walio pointi moja mbele yao na Newcastle ambao wako pointi mbili mbele ya Arsenal.
Kwa Man United, mbali ya kutaka kuing’oa kileleni Man City, wao pia wanataka kulipa kisasi kwa kufungwa bao 2-1 na Liverpool huko Anfield hivi karibuni na kutolewa kwenye FA Cup mechi ambayo wenyewe wanaamini fika hawakustahili kufungwa kwa jinsi walivyoitawala.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumapili Februari 12
Saa 10 na Nusu Jioni
Wolves v West Bromwich
Saa 1 Usiku
Aston Villa v Man City