Ligi Kuu England

BAADA KUSHINDA KESI: Redknapp akiri: ‘Lilikuwa Jinamizi baya!’

Jumatano, 08 Februari 2012 16:20
Chapisha Toleo la kuchapisha
  • ♦ Bosi wa Spurs adai Kesi haikupasa kutinga Mahakamani!

HARRY_REDKNAPP12Mara baada ya leo Mahakama kutoa hukumu kuwa hana kosa lolote katika mashitaka yaliyomkabili ya kukwepa kulipa Kodi, Meneja wa Tottenham Harry Redknapp amekiri kuwa kipindi chote cha Miaka mitano iliyopita alipokumbwa na tuhuma hizo kilikuwa ni kama Jinamizi baya kwake.

Baada ya Wazee wa Baraza la Mahakama kukaa Siku mbili wakitafakari Kesi iliyomkabili Redknapp na Mwenyekiti wa zamani wa Klabu ya Portsmouth, Milan Mandaric, Wazee hao walitoa kauli moja ya uamuzi kuwa wote wawili walikuwa hawana hatia yeyote kwenye mashitaka yao.

Mara baada ya kutoka Mahakamani baada ya kwisha Kesi hiyo iliyowagharimu Polisi Pauni Milioni 8 kuchunguza tuhuma za kuwa Mandaric alimwingizia Redknapp Pauni 189,000 kwenye Akaunti ya siri iliyobatizwa jina la Mbwa wa Redknapp Rosie huko Monaco ili kukwepa kulipa Kodi England, Redknapp amesisitiza Kesi hiyo haikupaswa kwenda Mahakamani.

Redknapp amesema: Ni Jinamizi. Ni Miaka mitano na Kesi hii haikupaswa kufika Mahakamani.’

Pia, Redknapp aliwashukuru Mawakili wake, Klabu na Mashabiki wa Tottenham pamoja na Familia yake kwa kumpa sapoti kubwa.

Maoni 

 
0 # Davie Wamara 2012-02-08 16:54
kesi ni kesi na tuhuma ni tuhuma na ukishinda kesi ktk tuhuma zinazokukabili ni muhim kufanya jambo kwa kufuata sheria
Reply | Reply with quote | Quote
 

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

adidas

All Originals 300x250

MATANGAZO

TANGAZA HAPA

SOKAINBONGO_BANNER1