Liverpool jana walishindwa kuwang’oa Arsenal kutoka nafasi ya 6 baada ya kwenda sare 0-0 na Tottenham katika mechi ya Ligi Kuu England iliyochezwa huko Anfield Jijini Liverpool.
Kwenye mechi hiyo, Straika wa Liverpool kutoka Uruguay, Luis Suarez, aliingizwa Kipindi cha Pili hiyo ikiwa mechi yake ya kwanza baada ya kumaliza kifungo chake cha mechi 8 alichopewa na FA kwa kumkashifu kibaguzi Beki wa Manchester United Patrice Evra lakini aliponea chupuchupu kukumbwa na balaa jingine dakika 3 tu baada ya kuingizwa alipomtimba tumboni Kiungo wa Tottenham Scott Parker na kupewa Kadi ya Njano badala ya Kadi Nyekundu ambayo wengi walitegemea.
Bosi wa Spurs, Harry Redknapp, ambae kwa Wiki mbili sasa amekuwa akishinda Mahakamani huko London kujitetea kwenye Kesi inayomkabili ya kukwepa kulipa kodi, hakuwepo Uwanjani baada ya kushindwa kusafiri kutoka London kufuatia Ndege yake aliyopangwa kusafiria kufutwa kutokana na ukungu mzito.
Vikosi:
Liverpool: Reina, Kelly, Skrtel, Agger, Johnson, Adam, Spearing, Kuyt, Gerrard, Bellamy, Carroll
Akiba: Doni, Aurelio, Suárez, Henderson, Coates, Downing, Carragher.
Tottenham: Friedel, Walker, Dawson, King, Assou-Ekotto, Parker, Livermore, Kranjcar, Modric, Bale, Adebayor
Akiba: Cudicini, Saha, Rose, Nelsen, Khumalo, Luongo, Lancaster.
Refa: Michael Oliver .
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Februari 11
Saa 9 Dak 45 Mchana
Manchester United v Liverpool
Saa 12 Jioni
Bolton Wanderers v Wigan Athletic
Sunderland v Arsenal
Blackburn Rovers v QPR
Swansea City v Norwich City
Everton v Chelsea
Fulham v Stoke City
Saa 2 na Nusu Usiku
Tottenham v Newcastle United
Februari 12
Saa 10 na Nusu Jioni
Wolves v West Bromwich
Saa 1 Usiku
Aston Villa v Man City
MSIMAMO:
[Timu zimecheza Mechi 24]
1 Man City Pointi Pointi 57
2 Man United 55
3 Tottenham 50
4 Chelsea 43
-----------------------------------
5 Newcastle 42
6 Arsenal 40
7 Liverpool 39
8 Sunderland 33
9 Norwich 32
10 Swansea 30
11 Everton 30
12 Stoke City 30
13 Aston Villa 28
14 Fulham 27
15 WBA 26
16 QPR 21
17 Wolves 21
--------------------------------
18 Bolton 20
19 Blackburn 18
20 Wigan 15
=========