RATIBA:
Jumatatu, 6 Februari 2012
[Saa 5 Usiku]
Liverpool v Tottenham
MSIMAMO Timu za juu:
[Timu zimecheza Mechi 24]
1 Man City Pointi Pointi 57
2 Man United 55
3 Tottenham [Mechi 23] 49
4 Chelsea 43
-----------------------------------
5 Newcastle 42
6 Arsenal 40
7 Liverpool [Mechi 23] 38
8 Sunderland 33
9 Norwich 32
10 Swansea 30
-----------------------------
Taarifa:
Liverpool wapo kwao Anfield kucheza mechi ya Ligi Kuu England wakiwinda ushindi ili kuipiku Arsenal nafasi ya 6 na kuzisakama Newcastle na Chelsea zilizo juu yao katika ile vita ya kumaliza katika Timu 4 za juu ili kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao lakini wapinzani wao wa leo ni Tottenham waliokamata nafasi ya 3 na ambao bado wana ndoto ya kuwa Bingwa kwa vile wako pointi 6 nyuma ya Manchester United walio nafasi ya pili na pointi 8 nyuma ya vinara Manchester City.
Leo Mchezaji wa Liverpool alietoka kifungo cha mechi 9, Luis Suarez, huenda akacheza na pia Nahodha wao Steven Gerrard pia huenda akacheza baada ya kupumzishwa mechi iliyopita.
Nao Tottenham huenda wakampa namba kwa mara ya kwanza Mchezaji wao mpya Louis Saha hasa kwa vile Mafowadi wao Jermaine Defoe, Emmanuel Adebayor na Rafael van der Vaart wana hatihati kwa kuwa na maumivu.
Mara ya mwisho Timu hizi kupambana ilikuwa Mwezi Septemba huko White Hart Lane na Liverpool kuchapwa mabao 4-0 lakini, mbali ya kuifunga Liverpool bao 2-0 Msimu uliopita Mwezi Mei Mwaka jana Uwanjani Anfield, Tottenham walikuwa hawajashinda hapo katika mechi zao 16 nyingine.
Lakini katika mechi zao 5 za mwisho kukutana, Liverpool wameshinda moja tu na kuchapwa 4.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Februari 11
Saa 9 Dak 45 Mchana
Manchester United v Liverpool
Saa 12 Jioni
Bolton Wanderers v Wigan Athletic
Sunderland v Arsenal
Blackburn Rovers v QPR
Swansea City v Norwich City
Everton v Chelsea
Fulham v Stoke City
Saa 2 na Nusu Usiku
Tottenham v Newcastle United
Februari 12
Saa 10 na Nusu Jioni
Wolves v West Bromwich
Saa 1 Usiku
Aston Villa v Man City