LIGI KUU ENGLAND

DABI ya Manchester yabadilishwa Ratiba!

Jumatano, 22 Februari 2012 17:32
Chapisha Toleo la kuchapisha

MAN_UNITED_TITLE_19Mechi 5 za Ligi za Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England, Manchester United, zilizokuwa zichezwe Mwezi Aprili zimepanguliwa na kupangiwa Ratiba upya ikiwemo ile Dabi kati ya Manchester City na Man United itakayochezwa Uwanja wa Etihad ili kukidhi matakwa ya Stesheni za TV ili kurusha mechi hizo laivu.

Dabi hiyo ya Manchester, ambayo awali ilikuwa ichezwe Aprili 28, sasa itachezwa Jumatatu Aprili 30 kuanzia Saa 4 Usiku, Bongo Taimu.

Mechi nyingine za Mabingwa hao zilizokumbwa na panga pangua hiyo ni pamoja na mechi za nyumbani dhidi ya QPR, Aston Villa na Everton.

Mechi nyingine iliyobadilishwa ni ile ya ugenini na Wigan.

Pia, mechi ya Man United Uwanjani Old Trafford hapo Jumamosi Machi 10 dhidi ya West Brom huenda ikabadilika ikiwa Man United watafuzu kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya EUROPA LIGI.

RATIBA Iliyobadilika kwa Aprili ni:

Jumapili Aprili 8

Man United v QPR [Saa 9 na Nusu Mchana]

Jumatano Aprili 11

Wigan v Man United [Saa 3 Dak 45 Usiku]

Jumapili Aprili 15

Man United v Aston Villa [Saa 12 Jioni]

Jumapili Aprili 22

Man United v Everton [Saa 8 na Nusu mchana]

Jumatatu Aprili 30

Man City v Man United [Saa 4 Usiku]

 

John Terry nje Miezi 2!

Jumanne, 21 Februari 2012 19:52
Chapisha Toleo la kuchapisha

Terry++Kuikosa mechi ya England v Holland, kutokutana na Rio England!

John Terry anatarajiwa kupasuliwa goti na hivyo kumweka nje ya uwanja kwa muda unaokadiriwa Miezi miwili.

Nahodha huyo wa Chelsea sasa atalikosa pambano dhidi ya Napoli litakalochezwa Jumanne usiku na pia kuchukuliwa kwenye Kikosi cha England ambacho kitacheza mechi ya kirafiki na Holland Wiki ijayo.

Terry aliumia goti lake walipoifunga Portsmouth Mwezi uliopita kwenye FA Cup na amezikosa mechi 4 za Chelsea, ambazo zote hawakushinda, lakini alitegemewa kucheza mechi na Napoli.

Hata hivyo, Terry alifanya mazoezi na wenzake jana lakini leo akalalamika ana maumivu kwenye goti ambalo limejaa maji.

Lakini kukosekana kwa Terry kuichezea England kunampunguzia kazi ngumu Kocha wa Muda Stuart Pearce ambae wengi wanahisi alikuwa na uamuzi mgumu wa kumchagua Terry na Rio Ferdinand pamoja baada ya Terry kuvuliwa Unahodha wa England kufuatia kukumbwa na tuhuma za kumtukana kibaguzi Mdogo wake Rio, Antoin Ferdinand, kwenye mechi kati ya Chelsea na QPR, na tuhuma hizo kumfikisha Terry Mahakamani ambako inategemewa kesi yake kuanza Mwezi Julai.

 

Torres ‘kupigwa shoka’ mechi na Napoli

Jumatatu, 20 Februari 2012 18:20
Chapisha Toleo la kuchapisha

TORRES12Fernando Torres, ambae ameigharimu Chelsea Pauni Milioni 50 Januari Mwaka jana na tangu wakati huo amefunga bao 3 tu za Ligi, huenda asicheze kabisa katika mechi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI ambayo Chelsea itacheza ugenini Jumanne huko Italia na Napoli katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano.

Majuzi Jumamosi, Torres alianza kwenye mechi ya FA Cup walipocheza na Birmigham Uwanjani Stamford Bridge na kutoka sare bao 1-1 lakini Torres alitolewa wakati wa haftaimu wakati wapo nyuma kwa bao 1-0 na nafasi yake kuchukuliwa na Didier Drogba na hatimaye Chelsea kusawazisha kwa bao la dakika ya 62 la Daniel Sturridge.

Ingawa Kocha wa Chelsea, Andre Villas-Boas, ambae nae yuko kwenye presha kubwa kwa kuboronga kwa Klabu yake Msimu huu, hajasema moja kwa moja Straika gani atacheza na Napoli lakini kidole kipo kwa Drogba ambae alipachika bao mara ya mwisho alipovaa Jezi ya Chelsea walipocheza na Aston Villa hapo Desemba 31 kabla kujiunga na Nchi yake Ivory Coast kwenye AFCON 2012 ambako aliifungia bao 3.

Mara ya mwisho kwa Torres kufunga bao ni Oktoba 19 alipoipatia Chelsea bao 2 walipoifunga Genk 5-0 kwenye mechi ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Kabla kujiunga na Chelsea Torres alikuwa Liverpool ambako alicheza mechi 102 na kufunga bao 65.

Kabla kujiunga na Chelsea Torres alikuwa Liverpool ambako alicheza mechi 102 na kufunga bao 65.

 

FA CUP: Arsenal yadundwa 2-0 nje!

Jumamosi, 18 Februari 2012 22:24
Chapisha Toleo la kuchapisha

WENGER-SITABWAGA_MANYANGAMATOKEO:

Jumamosi Februari 18

Chelsea 1 Birmingham 1 [Kurudiana huko St Andrew Stadium. Tarehe kupangwa]

Millwall 0 Bolton 2

Norwich 1 Leicester 2

Everton 2 Blackpool 0

Sunderland 2 Arsenal 0

TAARIFA:

Jumatano walinyukwa 4-0 na AC Milan na kuwekwa mguu mmoja nje ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na leo wametandikwa 2-0 na Sunderland na kutupwa nje ya FA Cup na sasa inaelekea wazi ule ukame wa Miaka 7 wa kukosa Taji lolote utaendelea maana hata kwenye Ligi Kuu England wako nafasi ya 4 na Pointi 17 nyuma ya vinara.

Bao za Sunderland leo zilifungwa na Kieran Richardson, Mchezaji wa zamani wa Manchester United, dakika ya 40 na Oxlade-Chamberlain kwa kujifunga mwenyewe mpira uliogonga posti na kurudi katika dakika ya 77.

RATIBA:

Jumapili Februari 19

[Saa 9 Mchana]

Crawley v Stoke

[Saa 11 Jioni]

Stevenage v Tottenham

[Saa 1 na Nusu Usiku]

Liverpool v Brighton

 

Wenger aomba radhi kipondo Milan, RVP ashauriwa kuhama Arsenal!

Jumamosi, 18 Februari 2012 14:09
Chapisha Toleo la kuchapisha

WENGER-SITABWAGA_MANYANGAWakati Meneja wa Arsenal Arsene Wenger akiomba radhi kwa Mashabiki wa Arsenal kufuatia kipigo chao cha mabao 4-0 huko Milan Jumatano iliyopita mikononi mwa AC Milan katika mechi ya kwanza ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, Straika wa AC Milan Zlatan Ibrahimovich amemshauri Nahodha wa Arsenal Robin van Persie kuhama Klabu hiyo ikiwa anataka kushinda Mataji.

Arsene Wenger, akiongea na Maripota hapo jana kabla ya safari ya Arsenal kwenda Stadium of Light kucheza na Sunderland Jumamosi katika mechi ya Raundi ya 5 ya FA Cup, amesema Mashabiki wao wamekuwa imara kwao na yeye hana budi kuomba radhi kwa matokeo mabovu.

Aliongeza: ‘Kesho ni siku nyingine na ni pambano jingine na tunataka watushangilie. Unaweza ukatoa zaidi ya sababu mia za kufungwa lakini ukweli ni kuwa tulicheza vibaya na haikuwa siku yetu!’

Sasa ni Miaka 7 tangu Arsenal watwae Taji na huku wakiwa mguu mmoja nje kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI na wapo nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England wakiwa Pointi 17 nyuma ya vinara Manchester City, FA Cup ndio imebaki njia kubwa kwao kutwaa Taji Msimu huu.

Wenger ametamka: ‘Kombe hili ni muhimu lakini kwa vile tulivunjwa moyo mechi iliyopita FA Cup imekuwa muhimu mno!’

RVP ashauriwa kuhama Arsenal

Robin van Persie ameshauriwa kuondoka Arsenal na Straika wa AC Milan Zlatan Ibrahimovic ambae ndie aliekuwa mwiba mkubwa baada ya Timu yake kuichapa Arsenal bao 4-0 Jumatano iliyopita.

Ibrahimovich ametamka: ‘Soka ni ushindi. Kama hushindi unataka kuondoka.’

Ibrahimovich aliongeza: ‘Nimeshinda Ubingwa mara 8 katika Miaka minane nikiwa na Klabu tofauti katika Nchi tofauti. Ukibweteke sehemu moja unajiona uko nyumbani na kila kitu rahisi tu. Ukihamia kwingine ni mtihani mkubwa. Ukishinda huko ndio unakuwa Bingwa wa kweli, na unaheshimika sana!’

 


Page 1 of 135

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2