News Items

EUROPA LIGI: Man City yaingia Raundi ijayo

Jumatano, 22 Februari 2012 22:25
Chapisha Toleo la kuchapisha

Wakicheza kwao Uwanja wa Etihad huku wakiwa na ushindi wa bao 2-1 walioupata ugenini huko Ureno Wiki iliyopita, Manchester City leo walijihakikishia kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada ya kuishindilia FC Porto, ambao walikuwa ndio Mabingwa watetezi wa Kombe hili, kwa bao 4-0.

Bao za Man City zilifungwa na Sergio Aguero, Edin Dzeko, David Silva na David Pizarro.

Katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 Man City wataanza kucheza ugenini na Mshindi kati ya Legia Warszawa ya Poland au Sporting Club ya Ureno ambao wanarudiana Alhamisi huko Ureno na matokeo ya mechi yao ya kwanza yalikuwa ni 2-2.

Katika Raundi hiyo ijayo Man City watamkosa Kiungo wao muhimu Yaya Toure kufuatia kupewa kwake Kadi ya Njano kwenye Dakika ya 65 katika mechi na FC Porto, hii ikiwa Kadi yake ya pili na hivyo kufungiwa mechi moja.

 

EUROPA LIGI: Man United kusonga?

Jumatano, 22 Februari 2012 21:23
Chapisha Toleo la kuchapisha

Man_United_v_AjaxManchester United v Ajax Amsterdam [Matokeo Mechi ya kwanza 2-0]

UWANJA: Old Trafford

SAA: 5 Dakika 5 Usiku

TAARIFA:

Manchester United Alhamisi usiku wanaikaribisha Ajax Amsterdam ya Uholanzi Uwanjani Old Trafford katika mechi ya marudiano ya Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya EUROPA LIGI baada ya kuifunga Ajax bao 2-0 huko Amsterdam ArenA Wiki iliyopita.

Mshindi wa mechi hii atapambana na Mshindi wa Mechi kati ya Athletic Bilbao na Lokomotiv Moscow kwenye Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na matokeo ya mechi ya Timu hizi katika mechi yao ya kwanza yalikuwa ni Lokomotiv Moscow 2 Athletic Bilbao 1 kwenye mechi iliyochezwa huko Urusi Wiki iliyopita.

HALI YA TIMU:

Baada ya kusuasua kwenye Msimu huu wa Ligi yao huko Uholanzi, Eredivisie, Ajax wamefanikiwa kushinda mechi yao ya pili mfululizo kwa kuichapa NEC Nijmegen bao 4-1 Wikiendi iliyopita.

Lakini, Ajax, wakiwa chini wa nguli wa Soka la Uholanzi, Frank De Boer, bila shaka, wanajua fika kuwa baada ya kuchapwa bao 2-0 huko kwao nafasi yao kusonga iko finyu katika mechi yao dhidi ya Man United Old Trafford.

Tangu mechi yao huko Amsterdam ArenA, Man United hawajacheza mechi yeyote kwa vile Wikiendi iliyopita kulikuwa ni mechi za FA Cup tu na wao walishatupwa nje ya michuano hiyo.

WACHEZAJI:

Staa wa Man United Wayne Rooney hatakuwepo kwa vile ni mgonjwa lakini Dimitar Berbatov huenda akacheza baada ya kupona maumivu huku kuna tetesi Kiungo chipukizi Paul Pogba huenda akapewa namba pamoja na kina Chris Smalling na Tom Cleverley.

Ajax itawakosa Nicolai Boilesen, Dmitry Bulykin na Theo Janssen lakini Beki wa zamani wa Blackburn, Andre Ooijer, anaweza kupewa namba.

REFA:

Damir Skomina ndie Mwamuzi na ndie aliechezesha mechi ambayo Napoli waliwafunga Manchester City 2-1 mapema Msimu huu kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI.

RATIBA:

[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]

Alhamisi Februari 23

[Saa 3 Usiku]

Athletic Bilbao v Lokomotiv Moscow [1-2]

PSV Eindhoven v Trabzonspor [2-1]

Standard Liege v Wisla Krakow [1-1]

Club Brugge v Hannover [1-2]

Valencia v Stoke City [1-0]

Twente v Steaua Bucharest [1-0]

Paok Salonika v Udinese [0-0]

Metalist Kharkiv v Red Bull Salzburg [4-0]

[Saa 5 Dak 5 Usiku]

Olympiakos v Rubin Kazan [1-0]

Manchester United v Ajax [2-0]

Atlético Madrid v Lazio [3-1]

Besiktas v Sporting Braga [2-0]

Anderlecht v AZ Alkmaar [0-1]

Sporting Lisbon v Legia Warsaw [2-2]

Schalke v Viktoria Plzen [1-1]

RAUNDI YA MTOANO TIMU 16:

Mechi kuchezwa Machi 8 na marudio Machi 15

[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]

FC Salzburg/Metalist Kharkiv v Rubin Kazan v Olympiacos

Legia Warszawa/Sporting Club v FC Porto/Manchester City

Steaua Bucuresti/FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

AZ Alkmaar/Anderlecht v Udinese/PAOK

Stoke City/Valencia v Trabzonspor/PSV Eindhoven

Ajax Amsterdam/Manchester United v Lokomotiv Moscow/Athletic Bilbao

Steaua Bucuresti /FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

Wisla Krakow/Standard Liege v Hannover 96/Brugge

 

DABI ya Manchester yabadilishwa Ratiba!

Jumatano, 22 Februari 2012 17:32
Chapisha Toleo la kuchapisha

MAN_UNITED_TITLE_19Mechi 5 za Ligi za Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England, Manchester United, zilizokuwa zichezwe Mwezi Aprili zimepanguliwa na kupangiwa Ratiba upya ikiwemo ile Dabi kati ya Manchester City na Man United itakayochezwa Uwanja wa Etihad ili kukidhi matakwa ya Stesheni za TV ili kurusha mechi hizo laivu.

Dabi hiyo ya Manchester, ambayo awali ilikuwa ichezwe Aprili 28, sasa itachezwa Jumatatu Aprili 30 kuanzia Saa 4 Usiku, Bongo Taimu.

Mechi nyingine za Mabingwa hao zilizokumbwa na panga pangua hiyo ni pamoja na mechi za nyumbani dhidi ya QPR, Aston Villa na Everton.

Mechi nyingine iliyobadilishwa ni ile ya ugenini na Wigan.

Pia, mechi ya Man United Uwanjani Old Trafford hapo Jumamosi Machi 10 dhidi ya West Brom huenda ikabadilika ikiwa Man United watafuzu kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya EUROPA LIGI.

RATIBA Iliyobadilika kwa Aprili ni:

Jumapili Aprili 8

Man United v QPR [Saa 9 na Nusu Mchana]

Jumatano Aprili 11

Wigan v Man United [Saa 3 Dak 45 Usiku]

Jumapili Aprili 15

Man United v Aston Villa [Saa 12 Jioni]

Jumapili Aprili 22

Man United v Everton [Saa 8 na Nusu mchana]

Jumatatu Aprili 30

Man City v Man United [Saa 4 Usiku]

 

KAMATI YA UCHAGUZI TFF—Yasimamisha Uchaguzi DRFA!

Jumatano, 22 Februari 2012 16:50
Chapisha Toleo la kuchapisha

Leo Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TFF, Deaogratias Lyatto, ametoa Taarifa kuhusu Uchaguzi wa Viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam, DRFA, kufuatia kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika tarehe 21 Februari 2012 kupitia mchakato wa Uchaguzi wa DRFA na ambacho pia kilijadili ushauri wa Kamati ya Sheria, Katiba na Hadhi kwa Wachezaji kuhusu Katiba ya DRFA.

NATIONAL_STADIUM2Taarifa hiyo inasema: ‘Kamati iliridhika na kukubaliana na ushauri wa Kamati ya Sheria, Katiba na Hadhi kwa Wachezaji kwamba Katiba ya DRFA haikidhi matakwa ya Katiba ya TFF.’

Taarifa hiyo iliendelea: ‘Kutokana na mapungufu ya msingi katika Ibara ya 29 na Ibara ya 30 ya Katiba ya DRFA, Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuzingatia Katiba ya TFF Ibara ya 49(1), Katiba ya DRFA Ibara ya 48, na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 26(2), Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kutumia mamlaka yake kikatiba na kikanuni imefuta uchaguzi wa DRFA uliokuwa ufanyike tarehe 18 Machi 2012. Mchakato wa Uchaguzi wa DRFA utaanza upya mara baada ya kukamilika marekebisho ya Vifungu vya Katiba ya DRFA vinavyokinzana na matakwa ya Katiba ya TFF kwa maelekezo ya Kamati ya Sheria, Katiba na Hadhi kwa Wachezaji, kabla ya tarehe 10 Agosti 2012.’

Taarifa hiyo ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilimalizia kwa kusema: ‘Kamati ya Uchaguzi ya TFF inatabaisha kuwa kwa kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF Ibara ya 2(4), uongozi wa DRFA utaendelea kuwa madarakani hadi hapo uchaguzi utakapofanyika kabla ya tarehe Agosti 2012 muda wao kuwa madarakani kikatiba utakapomalizika.’

 

EUROPA LIGI: Leo ni Man City v FC Porto

Jumatano, 22 Februari 2012 14:07
Chapisha Toleo la kuchapisha

EUROPA_LIGI_CUPRATIBA:

[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]

Jumatano Februari 22

[Saa 2 Usiku]

Manchester City v FC Porto [2-1]

TAARIFA:

Leo Uwanjani Etihad, Manchester City wanarudiana na FC Porto katika mechi ya EUROPA LIGI baada ya kuwachapa bao 2-1 huko Ureno Wiki iliyopita.

Mechi nyingine za EUROPA LIGI za marudiano zinachezwa kesho huku manchester United wakiwa kwao Old Trafford kucheza na Ajax Amsterdam ambao Wiki iliyopita waliwatwanga 2-0 huko Amsterdam ArenA.

Alhamisi Februari 23

[Saa 3 Usiku]

[Matokeo Mechi za kwanza kwenye mabano]

Athletic Bilbao v Lokomotiv Moscow [1-2]

PSV Eindhoven v Trabzonspor [2-1]

Standard Liege v Wisla Krakow [1-1]

Club Brugge v Hannover [1-2]

Valencia v Stoke City [1-0]

Twente v Steaua Bucharest [1-0]

Paok Salonika v Udinese [0-0]

Metalist Kharkiv v Red Bull Salzburg [4-0]

[Saa 5 Dak 5 Usiku]

Olympiakos v Rubin Kazan [1-0]

Manchester United v Ajax [2-0]

Atlético Madrid v Lazio [3-1]

Besiktas v Sporting Braga [2-0]

Anderlecht v AZ Alkmaar [0-1]

Sporting Lisbon v Legia Warsaw [2-2]

Schalke v Viktoria Plzen [1-1]

RAUNDI YA MTOANO TIMU 16:

Mechi kuchezwa Machi 8 na marudio Machi 15

[Timu inayotajwa kwanza ipo nyumbani]

FC Salzburg/Metalist Kharkiv v Rubin Kazan v Olympiacos

Legia Warszawa/Sporting Club v FC Porto/Manchester City

Steaua Bucuresti/FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

AZ Alkmaar/Anderlecht v Udinese/PAOK

Stoke City/Valencia v Trabzonspor/PSV Eindhoven

Ajax Amsterdam/Manchester United v Lokomotiv Moscow/Athletic Bilbao

Steaua Bucuresti /FC Twente v Viktoria Plzen/Schalke

Wisla Krakow/Standard Liege v Hannover 96/Brugge

 


Page 1 of 154

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2