DIMBANI AFRIKA

AWC 2012: Twiga Stars kucheza na Ethiopia

Jumanne, 31 Januari 2012 20:29
Chapisha Toleo la kuchapisha

TWIGA_STARS_TEAM_FOTOBaada ya kuichabanga Namibia kwa jumla ya mabao 7-2, Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania, Twiga Stars, itacheza na Ethiopia kwenye Raundi ya Kwanza ya michuano ya Kombe la Afrika kwa Wanawake ili kutafuta nafasi ya kuingia Fainali zake ambazo zitachezwa Mwezi Novemba huko Malabo Nchini Equatorial Guinea.

Ethiopia wamefuzu baada ya kuichapa Misri bao 4-0 na kuwatoa kwa jumla ya bao 6-4.

Mechi ya kwanza kati ya Twiga Stars na Ethiopia itachezwa huko Addis Ababa kati ya tarehe 25 hadi 27 Mei 2012 na marudiano ni Nchini Tanzania kati ya tarehe 15 hadi 17 Juni 2012.

MATOKEO KAMILI Mechi za Raundi ya Awali:

Ghana 5 Mali 0

*Ghana wamesonga kwa jumla ya Mabao 8-0

Tanzania 5 Namibia 2

*Tanzania wamesonga kwa bao 7-2

Guinea 0 Cote d’Ivoire 5

*Cote d’Ivoire wamepita kwa bao 10-1

Ethiopia 4 Egypt 0

*Ethiopia wamesonga kwa bao 6-4

Malawi 4 Zambia 2

*Zambia wameshinda jumla ya bao 9-4

Zimbabwe 2 Botswana 1

*Zimbabwe wamepita kwa bao 3-1

DR Congo 4 Uganda 0

*DR Congo wamesonga kwa bao 5-1

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

adidas

All Originals 300x250

MATANGAZO

TANGAZA HAPA

SOKAINBONGO_BANNER1