MSIMAMO Timu za juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 16]
1 Yanga Pointi 34 [Bao za kufunga 28, kufungwa 13, tofauti ya Magoli 15]
2 Simba Pointi 34 [Bao za kufunga 25, kufungwa 10, tofauti ya Magoli 15]
3 Azam Pointi 32
3 JKT Oljoro Pointi 26
5 Mtibwa Sugar Pointi 22
Taarifa:
Huko Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Vodacom, Yanga, wamefanikiwa kuongoza Ligi kwa kuipiku Simba kwa tofauti ya magoli baada ya kuichapa Mtibwa Sugar kwa mabao 3-1.
Yanga na Simba zote zimelingana kwa Pointi wakiwa na Pointi 34 kwa mechi 16 na tofauti ya magoli 15 kwa kila mmoja lakini Yanga wako juu kwa kuwa na bao nyingi za kufunga, bao 28 dhidi ya bao 25 za Simba.
Katika mechi ya leo bao za Yanga zilifungwa na Asamoah, Kiiza na Shamte.
RATIBA:
Jumamosi Februari 11
Coastal Union v African Lyon
JKT Oljoro v JKT Ruvu
Polisi Dodoma v Villa Squad
Simba v Azam
Toto African v Moro United
Jumapili Februari 12
Kagera Sugar v Mtibwa Sugar
Yanga v Ruvu Shooting
Jumanne Februari 14
Polisi Dodoma v Simba
Yanga v African Lyon