Bongo Nyuzi

Makocha Yanga, Simba waweweseka na Vikosi vyao!

Jumanne, 17 Januari 2012 10:03
Chapisha Toleo la kuchapisha

YANGA_V_SIMBA11Makocha wa Klabu kongwe Nchini, Yanga na Simba, ambao Timu zao zinakabiliwa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaoanza hapo Januari 21 na pia Mashindano ya Klabu za Afrika Mwezi Februari, wameonyesha kutoridhika na Vikosi vyao wakati wakijifua kwa michuano hiyo.

Kocha wa Simba, Milovan Cirkovic, amekaririwa akisema kiwango cha Timu yake na hasa safu ya ulinzi bado hakiridhishi.

Majuzi Simba walitoka sare 1-1 na Tusker ya Kenya na Cirkovic alionekana kutofurahishwa na uchezaji wa Timu yake.

Simba inatarajiwa kucheza michuano ya Afrika ya Kombe la Shirikisho ugenini Kigali, Rwanda ambapo itamenyana na Kiyovu ya huko Februari 18 katika mechi ya kwanza.

Nae Kocha wa Yanga, Kostadin Papic, ameponda matayarisho ya Timu kwa kukumbwa na kuvunjika kwa mazoezi na kambi yao kukabiliwa na matatizo mengi.

Ingawa Jumamosi iliyopita Yanga ilifanikiwa kuifunga Sofapaka ya Kenya mabao 2-1, matokeo hayo hayakumpa moyo Papic ambae ameonya maandalizi hafifu hayawezi kumfanya atoe ahadi ya Ubingwa wa Ligi na kuifunga Zamalek hapo Februari 18 watakapocheza katika mechi ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika.

Kutoa maoni

Tafadhali toa maoni sahihi kwa kutumia lugha ya heshima.


Security code
Onyesha tena

Ingia

Jiandikishe / Ingia

MATANGAZO

TANGAZA_BURE2