DABI ya KARIAKOO-SIMBA v YANGA: SIMBA CHALIIIII!!!
>>MABINGWA YANGA 2 SIMBA 0!!
MABINGWA wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, Yanga, leo wamemaliza Msimu wa 2012/13 kwa furaha kubwa baada ya kuwatandika Wapinzani wao wa Jadi Simba kwa Bao 2-0 katika Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Yanga, ambao waliutwaa Ubingwa mapema wakiwa na Mechi kadhaa mkononi, walianza Mechi hii kwa kishindo na Didier Kavumbagu ndie alieanza sherehe za kupokea Kombe la Ubingwa mapema alipofunga Bao katika Dakika ya 4 tu.
Simba walipata nafasi murua ya kusawazisha Bao hilo katika Dakika ya 28 walipopewa Penati kufuatia Nadir Haroub 'Cannavaro' kumuangusha Mrisho Ngassa lakini Mussa Mudde akakosa Penati hiyo.
Hadi Mapumziko Yanga 1 Simba 0.
Kipindi cha Pili, Dakika ya 63, Hamis Kiiza alifungia Yanga Bao la Pili.
Mechi hii nusura iingie hitilafu katika Dakika ya 89 baada ya Cholo wa Simba na Kavumbagu kuvaana na Refa Martin Saanya alipoingilia kati akaanguka na alipoinuka alionekana kutokwa damu lakini Mechi iliendelea.
Hii ni mara ya Pili Timu hizi kukutana Msimu huu kweye VPL na mara ya kwanza matokeo yalikuwa Bao 1-1 hapo Oktoba 3, 2012.
VIKOSI:
Yanga: Ally Mustapha 'Barthez', Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondan, Athuman Idd 'Chuji', Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza, Haruna Niyonzima
Akiba: Said Mohamed, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nurdin Bakar, Nizar Khalfan, Said Bahanuz, Jerry Tegete
Simba: Juma Kaseja, Nassor Masoud 'Chollo', Haruna Shamte, Shomari Kapombe, Mussa Mudde, William Lucian, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba, Haruna Chanongo
Akiba: Abel Dhaira, Miraji Adam, Ramadhan Singano 'Messi', Felix Sunzu, Christopher Edward, Jonas Mkude, Hassan Mkude
REFA: Martin Saanya [Morogoro]
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi Mei 18
Simba SC 0 Yanga 2
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
***YANGA+++BINGWA
|
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
|
1
|
YANGA
|
26
|
18
|
6
|
2
|
47
|
14
|
33
|
60
|
|
2
|
AZAM FC
|
25
|
15
|
6
|
4
|
45
|
20
|
25
|
51
|
|
3
|
SIMBA SC
|
26
|
12
|
9
|
5
|
38
|
25
|
13
|
45
|
|
4
|
KAGERA SUGAR
|
25
|
11
|
8
|
6
|
26
|
19
|
7
|
41
|
|
5
|
MTIBWA SUGAR
|
25
|
10
|
9
|
6
|
29
|
24
|
5
|
39
|
|
6
|
COASTAL UNION
|
25
|
8
|
11
|
6
|
25
|
23
|
2
|
35
|
|
7
|
RUVU SHOOTING
|
25
|
8
|
8
|
9
|
22
|
24
|
-2
|
32
|
|
8
|
JKT OLJORO
|
25
|
7
|
8
|
10
|
21
|
26
|
-5
|
29
|
|
9
|
TANZANIA PRISONS
|
25
|
7
|
8
|
10
|
16
|
22
|
-6
|
29
|
|
10
|
JKT RUVU
|
25
|
7
|
5
|
13
|
21
|
38
|
-17
|
26
|
|
11
|
MGAMBO SHOOTING
|
25
|
7
|
4
|
14
|
16
|
27
|
-11
|
25
|
|
12
|
POLISI MOROGORO
|
25
|
4
|
10
|
11
|
13
|
23
|
-10
|
22
|
|
13
|
TOTO AFRICAN
|
25
|
4
|
10
|
11
|
21
|
33
|
-12
|
22
|
|
14
|
AFRICAN LYON
|
25
|
5
|
4
|
16
|
16
|
38
|
-22
|
19
|
***AFRICAN LYON IMESHUKA DARAJA
WAOWAHI KUWA MABINGWA:
1965 Sunderland (Sasa inaitwa Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans
|
LEO DABI ya KARIAKOO: YANGA v SIMBA, NANI MBABE??
>>BRANDTS: “BILA KUIFUNGA SIMBA, UBINGWA HAUNOGI!!”
>>LIEWIG: “TUNAJUA YANGA BINGWA ILA KUMFUNGA LAZIMA!”
LEO UWANJA WA TAIFA, DAR ES SALAAM utafurika umati wa Mashabiki wa Klabu Kongwe Nchini kushuhudia pambano la mwisho la Msimu huu wa VPL, Ligi Kuu Vodacom, kati ya Mabingwa Yanga na Mahasimu wao wakubwa Simba, hii ikiwa ni ‘Dabi ya Kariakoo’.
Mbali ya Mechi hii ya Yanga na Simba Timu nyingine 12 zitacheza Mechi zao za mwisho pia hii leo huku mtanange ni kuzipata Timu 2, kati ya Mgambo Shooting, Polisi Morogoro na Toto Afrcans, ambazo zitaungana African Lyon kushuka Daraja.
Ukiondoa kulinda hadhi, pambano hili ni la kukamilisha Ratiba tu kwa vile Yanga ndie Bingwa na Simba wao wamekamata nafasi ya 3 huku nafasi ya Pili ikichukuliwa na Azam FC.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
TAARIFA ZA TIKETI
MECHI: Jumamosi Mei 18 Kuanzia Saa 10 Jioni
Vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.
Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Lakini Siku zote pambano hili ni la kutambiana na hasa ukichukulia matokeo ya hivi karibuni hasa ule usongo wa Yanga kulipiza kisasi baada ya kuchapwa 5-0 na Sima Msimu uliopita.
Safari hii Wadau wa Yanga wanahisi nafasi ndio yao kwani Simba hivi karibuni ilichukua uamuzi mgumu wa kuwatema Wachezaji wao wazoefu kina Haruna Moshi ‘Boban’, Juma Nyosso na Amir Maftah na kuwachezesha Chipukizi, ambao hata hivyo, wameonyesha umahiri mkubwa.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
REKODI:
LIGI KUU: Ushindi Yanga 37 Simba 32 Sare 31
UBINGWA: Yanga 23 Simba 18
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Timu zote hizi zilipiga Kambi zao huko Visiwani Unguja kwa Yanga, chini ya Kocha wao toka Uholanzi Ernie Brandts, kuwa Pemba, na Simba, chini ya Mfaransa, Patrick Liewig, kutua huko Zanzibar.
Hii ni mara ya Pili Timu hizi kukutana Msimu huu kweye VPL na mara ya kwanza matokeo yalikuwa Bao 1-1 hapo Oktoba 3, 2012.
Akiongelea Mechi hii, Kocha wa Yanga, Ernie Brandts, amesema: “Bila kuifunga Simba Ubingwa haunogi na ndio maana tumejizatiti ili kupata ushindi!”
Nae Liewig wa Simba alisema: “Tunajua Yanga ni Bingwa lakini sisi kama Simba tutahakikisha tunashinda!.”
Mwamuzi wa Mechi hii ni Martin Saanya kutoka Morogoro atakaesaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha na Jesse Erasmo kutoka Morogoro.
Mwamuzi wa Akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam na Kamishna wa Mechi ni Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati Mtathmini wa Waamuzi (Referees Assessor) ni Leslie Liunda.
VIKOSI:
YANGA: Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbage, Hamis Kiiza
SIMBA: Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Miraj Adam, Mussa Mudde, Shomary Kapombe, Jonas Mkude, Mrisho Ngassa, Mwinyi Kazimoto, Ramadhani Singano, Amri Kiemba na Chanongo.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi Mei 18
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
***YANGA+++BINGWA
|
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
|
1
|
YANGA
|
25
|
17
|
6
|
2
|
45
|
14
|
31
|
57
|
|
2
|
AZAM FC
|
25
|
15
|
6
|
4
|
45
|
20
|
25
|
51
|
|
3
|
SIMBA SC
|
25
|
12
|
9
|
4
|
38
|
23
|
15
|
45
|
|
4
|
KAGERA SUGAR
|
25
|
11
|
8
|
6
|
26
|
19
|
7
|
41
|
|
5
|
MTIBWA SUGAR
|
25
|
10
|
9
|
6
|
29
|
24
|
5
|
39
|
|
6
|
COASTAL UNION
|
25
|
8
|
11
|
6
|
25
|
23
|
2
|
35
|
|
7
|
RUVU SHOOTING
|
25
|
8
|
8
|
9
|
22
|
24
|
-2
|
32
|
|
8
|
JKT OLJORO
|
25
|
7
|
8
|
10
|
21
|
26
|
-5
|
29
|
|
9
|
TANZANIA PRISONS
|
25
|
7
|
8
|
10
|
16
|
22
|
-6
|
29
|
|
10
|
JKT RUVU
|
25
|
7
|
5
|
13
|
21
|
38
|
-17
|
26
|
|
11
|
MGAMBO SHOOTING
|
25
|
7
|
4
|
14
|
16
|
27
|
-11
|
25
|
|
12
|
POLISI MOROGORO
|
25
|
4
|
10
|
11
|
13
|
23
|
-10
|
22
|
|
13
|
TOTO AFRICAN
|
25
|
4
|
10
|
11
|
21
|
33
|
-12
|
22
|
|
14
|
AFRICAN LYON
|
25
|
5
|
4
|
16
|
16
|
38
|
-22
|
19
|
***AFRICAN LYON IMESHUKA DARAJA
WAOWAHI KUWA MABINGWA:
1965 Sunderland (Sasa inaitwa Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans
DABI YA KARIAKOO: SHANGWE JANGWANI AU MSIMBAZI???
>> VPL: BINGWA YANGA KUIBAMIZA SIMBA ‘MDEBWEDO’??
>>MGAMBO, POLISI, TOTO, 2 ZIPI KUIFUATA LYON CHINI??
VPL, LIGI KUU VODACOM, inafika tamati Jumamosi Mei 18 wakati tayari Bingwa ni Yanga, Mshindi wa Pili ni Azam FC na kilichobaki ni Timu zipi mbili zitaungana na African Lyon kucheza FDL Msimu ujao lakini bado BIGI MECHI ni ile ile DABI ya KARIAKOO kati ya Yanga na Simba.
Siku zote ni Bigi Mechi Yanga na Simba lakini safari hii ‘kachumbari’ hamna maana tayari Yanga ni Bingwa na Nafasi ya Pili imechukuliwa na Azam FC na Simba watabaki Nafasi ya Tatu tu, na hivyo kutocheza Klabu Afrika Msimu ujao, lakini Siku zote Mechi hii ni ya ushindani uliojaa kila majigambo, sifa na hekaheka kila Kona ya Dar es Salaam na Nchi nzima.
Hii ndio DABI ya KARIAKOO, Mechi tangu zama za zamani ina vituko, shamrashamra na kila aina ya vioja.
Na ndio maana Timu zote, Yanga na Simba, zilipiga Kambi nje ya Dar es Salaam huko Visiwani Unguja, kwa Yanga, chini ya Kocha wao toka Uholanzi Ernie Brandts, kuwa Pemba, na Simba, chini ya Mfaransa, Patrick Liewig, kutua huko Zanzibar.
Hii ni mara ya Pili Timu hizi kukutana Msimu huu kweye VPL na mara ya kwanza matokeo yalikuwa Bao 1-1 hapo Oktoba 3, 2012.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUMBUKUMBU TU-3 OKTOBA 2012:
YANGA 1 SIMBA 1
Simba ndio walitangulia kupata bao Dakika ya 4 tu ya mchezo kwa bao la Amri Kiemba baada ya kupokea pande zuri toka kwa Mwinyi Kazimoto.
Hadi mapumziko Simba walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Yanga walisawazisha bao kwa Penati katika Dakika ya 66 baada ya Ngalema kuunawa mpira na Penati hiyo kufungwa na Saidi Bahanuzi.
Baada ya hapo Yanga walipata pigo baada ya Chipukizi wao Simon Msuva kupewa Kadi Nyekundu kwa kumpiga Juma Nyosso.
Matokeo haya yameifanya Simba iwe na Pointi 13 kwa Mechi 5 na Yanga kuwa na Pointi 8 kwa idadi hiyo hiyo ya Mechi.
VIKOSI:
SIMBA: Juma Kaseja, Nassor Chollo, Paul Ngalema, Juma Nyosso, Shomary Kapombe, Amri Kiemba, Edward Christopher, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Mrisho Ngassa.
Akiba: Wilbert Mweta, Komabil Keta, Paschal Ochieng, Kiggi Makassy, Salum Kinje, Daniel Akuffo, Abdallah Juma na Ramadhan Chombo ‘Redondo’
YANGA: Yaw Berko, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Cannavaro, Kevin Yondan, Athumani Iddi, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbangu, Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza.
Akiba: Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, Godfrey Taita, Stafano Mwasyika, Job Ibrahim, Frank Domayo, Nizar Khalfan, Shamte Ally, Idrisa Rajab na Jerry Tegete.
Refa: Mathew Akrama
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi Mei 18
Toto Africans Vs Ruvu Shooting
Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Polisi Moro Vs Coastal Union
MSIMAMO:
***YANGA+++BINGWA
|
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
PTS
|
|
1
|
YANGA
|
25
|
17
|
6
|
2
|
45
|
14
|
31
|
57
|
|
2
|
AZAM FC
|
25
|
15
|
6
|
4
|
45
|
20
|
25
|
51
|
|
3
|
SIMBA SC
|
25
|
12
|
9
|
4
|
38
|
23
|
15
|
45
|
|
4
|
KAGERA SUGAR
|
25
|
11
|
8
|
6
|
26
|
19
|
7
|
41
|
|
5
|
MTIBWA SUGAR
|
25
|
10
|
9
|
6
|
29
|
24
|
5
|
39
|
|
6
|
COASTAL UNION
|
25
|
8
|
11
|
6
|
25
|
23
|
2
|
35
|
|
7
|
RUVU SHOOTING
|
25
|
8
|
8
|
9
|
22
|
24
|
-2
|
32
|
|
8
|
JKT OLJORO
|
25
|
7
|
8
|
10
|
21
|
26
|
-5
|
29
|
|
9
|
TANZANIA PRISONS
|
25
|
7
|
8
|
10
|
16
|
22
|
-6
|
29
|
|
10
|
JKT RUVU
|
25
|
7
|
5
|
13
|
21
|
38
|
-17
|
26
|
|
11
|
MGAMBO SHOOTING
|
25
|
7
|
4
|
14
|
16
|
27
|
-11
|
25
|
|
12
|
POLISI MOROGORO
|
25
|
4
|
10
|
11
|
13
|
23
|
-10
|
22
|
|
13
|
TOTO AFRICAN
|
25
|
4
|
10
|
11
|
21
|
33
|
-12
|
22
|
|
14
|
AFRICAN LYON
|
25
|
5
|
4
|
16
|
16
|
38
|
-22
|
19
|
***AFRICAN LYON IMESHUKA DARAJA
WAOWAHI KUWA MABINGWA:
1965 Sunderland (Sasa inaitwa Simba SC)
1966 Sunderland
1967 Cosmopolitan
1968 Young Africans
1969 Young Africans
1970 Young Africans
1971 Young Africans
1972 Young Africans
1973 Simba SC
1974 Young Africans
1975 Mseto SC
1976 Simba SC
1977 Simba SC
1978 Simba SC
1979 Simba SC
1980 Simba SC
1981 Young Africans
1982 Pan Africans
1983 Young Africans
1984 Simba SC
1985 Young Africans
1986 Tukuyu Stars
1987 Young Africans
1988 Coastal Union
1989 Young Africans
1990 Simba SC
1991 Young Africans
1992 Young Africans
1993 Young Africans
1994 Simba SC
1995 Simba SC
1996 Young Africans
1997 Young Africans
1998 Young Africans
1999 Mtibwa Sugar
2000 Mtibwa Sugar
2001 Simba SC
2002 Young Africans
2003 Simba SC
2004 Simba SC
2005 Young Africans
2006 Young Africans
2007 Simba SC
2007/08 Young Africans
2008/09 Young Africans
2009/2010 Simba SC
2010/2011 Young Africans
2011/2012 Simba SC
2012/2013 Young Africans
KIM ATAJA 26 STARS WA KUIVAA MOROCCO
>> TANZANIA YAJITOA MICHUANO YA COSAFA
>> TIKETI SIMBA, YANGA KUANZA KUUZWA KESHO
>>TIKETI NI KUANZIA SH. 5,000 HADI 30,000
PATA HABARI KAMILI:
Release No. 084
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 16, 2013
KIM ATAJA 26 STARS WA KUIVAA MOROCCO
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen leo (Mei 16 mwaka huu) ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.
Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku akiacha wengine watatu aliokuwa nao kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Morocco ambapo Taifa Stars ilishinda mabao 3-1.
Wapya aliowaita katika kikosi hicho kitakachoingia kambini Mei 20 mwaka huu, saa 1 jioni kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam ni Ally Mustafa, Vicent Barnabas, Juma Luzio, Haruna Chanongo, Mudhathiri Yahya na Zahoro Pazi. Wachezaji aliowaacha ni Shabani Nditi, Nassoro Masoud Cholo na Issa Rashid.
Kikosi kamili cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kabla ya kwenda Morocco kitapita jijini Addis Ababa, Ethiopia kucheza mechi ya kirafiki Juni 2 mwaka huu dhidi ya Sudan ni kama ifuatavyo;
Makipa ni nahodha Juma Kaseja (Simba), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar) na Waziri Salum (Azam).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mudathiri Yahya (Azam) na Salum Abubakar (Azam).
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Juma Luzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Zahoro Pazi (JKT Ruvu).
Kocha Kim amesema kikosi kitakachoingia kambini kitakuwa na wachezaji 24 ambapo Samata na Ulimwengu watajiunga na timu jijini Marrakech, lakini wachezaji atakaondoka nao Dar es Salaam kwenda Addis Ababa ni 22 ambapo ataacha kipa mmoja na mchezaji mmoja wa ndani.
Awali TFF ilikuwa imeitafutia Taifa Stars mechi ya kirafiki Juni 1 mwaka huu dhidi ya Algeria, Libya au Misri. Lakini baadaye Algeria ikasema itacheza na Togo, wakati Misri ilitaka mechi hiyo ichezwe Juni 4 jijini Cairo, jambo ambalo lisingewezekana kwa Stars kwani ina mechi ya mashindano Juni 8 mwaka huu.
Kwa upande wa Libya mechi hiyo ilikubaliwa ichezwe Tunis, Tunisia, Juni 2 mwaka huu. Lakini baadaye Libya ikataka mechi hiyo ichezewe jijini Tripoli ambapo TFF ilikataa kutokana na sababu za kiusalama.
TANZANIA YAJIONDOA MICHUANO YA COSAFA
Tanzania (Taifa Stars) imejitoa kwenye michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika nchini Zambia kuanzia Julai 2-26 mwaka huu.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah amesema Stars ambayo iliingizwa katika michuano hiyo kama timu mwalikwa imejitoa kutokana na mwingiliano wa ratiba kati ya michuano hiyo na mechi za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).
Amesema awali Tanzania ilithibitisha kushiriki michuano kwa matarajio kwamba Uganda ingekubali ombi la TFF la kubadilisha ratiba ya mechi za CHAN, lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) likagoma kwa vile kipindi ambacho kilipendekezwa lenyewe litakuwa na uchaguzi wa viongozi wao.
Taifa Stars itacheza na Uganda (The Cranes) katika mechi za CHAN ambapo mechi ya kwanza itachezwa jijini Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu wakati ya marudiano itafanyika jijini Kampala kati ya Julai 26-28 mwaka huu.
Akizungumzia michuano ya COSAFA, Kocha Kim amesema angependa kushiriki michuano hiyo kwani ingekuwa kipimo kizuri kwa kikosi chake, lakini kwa sasa malengo makubwa ya Stars kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ambayo fainali zake zitafanyika mwaka 2015.
TIKETI SIMBA, YANGA KUANZA KUUZWA KESHO
Tiketi kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.
Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
YANGA v SIMBA-MEI 18: KIINGILIO 5,000/=, MWAMUZI ATAJWA!
>> UFAFANUZI KUHUSU LIGI YA MABINGWA MIKOA
>> KOCHA KIM KUZUNGUMZIA MECHI YA MOROCCO
PATA HABARI KAMILI:
UFAFANUZI KUHUSU LIGI YA MABINGWA MIKOA
Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) ilianza tarehe 12 Mei 2013 ikishirikisha klabu bingwa za mikoa yote ya Tanzania Bara, isipokuwa mikoa ya Pwani na Manyara ambayo kutokana na sababu tofauti ilishindwa kuwasilisha majina ya klabu zake hadi siku ya mwisho iliyowekwa na Kamati ya Mashindano, yaani tarehe 10 Mei 2013.
Suala la kukosekana kwa wawakilishi wa mikoa hiyo miwili limezua maswali mengi kiasi kwamba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linalazimika kutoa ufafanuzi kwa faida ya wadau wote wa mpira wa miguu.
Ligi ya Mabingwa wa Mikoa, ambayo ni mpya baada ya TFF kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa mpira wa miguu, ilipangwa kuanza tarehe 5 Mei 2013, lakini hadi tarehe ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, yaani tarehe 2 Mei 2013 mikoa michache ndiyo iliyokuwa imemaliza ligi zao na kupata mabingwa.
Kuchelewa huko kwa mikoa kumaliza ligi zao kuliilazimisha Kamati ya Mashindano ya TFF kuongeza muda wa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi hao hadi tarehe 10 Mei 2013 na hivyo siku ya kuanza kwa Ligi kusogezwa mbele hadi tarehe 12 Mei 2013.
Hadi kufikia tarehe hiyo mpya ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, ni mikoa sita tu iliyofaidika na kuongezwa huko kwa muda na kupata wawakilishi wake. Mikoa hiyo ni Iringa, ambayo pamoja na kuongezwa kwa muda, iliandika barua ya kuihakikishia Kamati ya Mashindano kuwa itapata bingwa kabla ya kuisha kwa siku ya tarehe 10 Mei 2013.
Mikoa mingine ni Lindi, Mtwara, Geita, Tabora na Dodoma.
Mkoa wa Manyara haukuweza kumaliza ligi yake hadi mwisho wa siku ya tarehe 10 Mei 2013 na hivyo Kamati ya Mashindano iliyosubiri majina hadi saa 12:00 jioni siku hiyo kuamua kuwaondoa wawakilishi wa Manyara kwenye ratiba.
Awali, Kamati ya Mashindano iliamua kuwa ratiba ya mechi za Ligi ya Mabingwa wa Mikoa ipangwe tarehe 7 Mei 2013, ikishirikisha mikoa ambayo ilishapata mabingwa wake, lakini baada ya kuona baadhi ya mikoa ilikuwa haijakamilisha ligi zake, Kamati iliamua kuwa ratiba ipangwe kwa kutumia majina ya mikoa kwa matumaini kuwa hadi kufikia tarehe 10 Mei 2013, mikoa itakuwa imeshapata wawakilishi wake na kwa kuwa ratiba inahusu mikoa jirani, ingekuwa rahisi kwa timu kusafiri kutoka kituo kimoja hadi kingine.
Lakini Mkoa wa Manyara haukuweza kufanya hivyo na Kamati kulazimika kuuondoa kwenye ratiba kutokana na kushindwa kukidhi utashi huo.
Mkoa mwingine ambao uliondolewa kwenye ratiba ni Pwani ambayo pamoja na kutuma jina la mwakilishi wake, Kamati ilipokea malalamiko kutoka klabu zilizoshiriki Ligi ya Mkoa, zikidai kuwa jina la bingwa wa Pwani lililowasilishwa TFF lilikuwa batili kwa kuwa klabu ya Kiluvia United haikustahili kushiriki Ligi ya Mkoa kutokana na ukweli kuwa haijasajiliwa mkoani Pwani na wala haikushiriki ligi ya mkoa msimu uliopita. Kamati ya Mashindano iliiondoa Pwani kwenye ratiba na kulirudisha suala hilo mkoani.
Ingawa Katibu wa Pwani alijaribu kuishawishi Sekretarieti ya TFF iliangalie suala hilo kwa undani zaidi, Sekretarieti ilimjibu kuwa lilishafanyiwa uamuzi na Kamati, hivyo uamuzi huo usingeweza kutenguliwa na kumshauri katibu huyo arejee mkoani kwake kuwasiliana na viongozi wenzake kuona ni jinsi gani mkoa unaweza kunusuru hali hiyo kwa kufanya uamuzi ambao ungeuwezesha mkoa kupata mwakilishi.
Kwa mantiki hiyo, masuala ya Manyara na Pwani yalikuwa ndani ya uongozi wa mikoa husika na si Kamati ya Mashindano ya TFF kwa kuwa Kamati ilitaka ipatiwe jina la bingwa ambaye alipatikana kwa mujibu wa mfumo mpya wa Ligi ya Mikoa.
Ligi ya Mabingwa wa Mikoa inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na hivyo timu zilizokutana tarehe 12 Mei 2013, zitarudiana mwishoni mwa wiki hii na kupatikana timu zitakazosonga mbele kwenye raundi nyingine hadi timu tatu bora zitakazopanda daraja kwenda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakapopatikana.
Ligi za Mikoa, kwa mujibu wa kanuni mpya, zinatakiwa ziwe na timu kati ya 16 na 20 na zinatakiwa zicheze mechi mbili za nyumbani na ugenini, hata kama zitakuwa zinatumia uwanja mmoja.
Uamuzi wa kubadilisha mfumo huo ulifanywa ili kuhakikisha kuwa mikoa inakuwa na na mashindano kwa mwaka mzima na hivyo kuiwezesha mikoa kujikita katika kutafuta mbinu za kupata fedha na kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu kwenye mikoa yao.
Uamuzi huo pia unasaidia kupunguza mtindo wa wachezaji kuzunguka klabu tofauti katika msimu mmoja kwa kuwa wanalazimika kutulia kwenye klabu moja hadi muda wa usajili unapofika.
Pamoja na wachezaji kutulia sehemu moja kwa muda mrefu, pia walimu wanapata fursa ya kujikita vizuri kwenye programu zao kwa kuwa wanakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya wachezaji wao.
Pamoja na hayo yote, mfumo huo utasaidia kurudisha msisimko kwenye mikoa na hivyo kutoa fursa kwa vijana wengi wenye vipaji kuonekana na kuendelezwa.
TFF inatoa wito kwa viongozi wa mikoa kuanza kubuni sasa mikakati ya kuendesha ligi hizo msimu unaokuja kwa kuwa hakutakuwa na nafasi tena ya kuongeza muda kwa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi wao.
KIINGILIO MECHI YA SIMBA, YANGA 5,000/-
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.
Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.
Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.
Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.
KOCHA KIM KUZUNGUMZIA MECHI YA MOROCCO
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya tiketi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco. Mkutano huo utafanyika keshokutwa (Mei 16 mwaka huu) saa 5 kamili kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
|
|